-
Usitawi wa Muundo wa TengenezoMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Hatua ya maana sana kuelekea kusahihishwa kwa hali hiyo ilichukuliwa katika 1919 gazeti The Golden Age lilipoanza kutangazwa. Hilo lingekuwa kifaa chenye nguvu cha kutangaza Ufalme wa Mungu kuwa utatuzi pekee wenye kudumu kwa matatizo ya wanadamu. Kila kutaniko ambalo lilitaka kushiriki katika utendaji huo lilialikwa liombe kwamba lisajiliwe na Sosaiti kuwa “tengenezo la utumishi.” Halafu mwelekezi, au mwelekezi wa utumishi kama alivyokuja kujulikana, ambaye hakulazimika kuchaguliwa kila mwaka, aliwekwa na Sosaiti.f Akiwa ndiye mwakilishi wa Sosaiti mwenyeji, alipaswa kupanga kazi, kutoa migawo ya eneo, na kutia kutaniko moyo lishiriki katika utumishi wa shambani. Hivyo, sambamba na wazee na mashemasi waliochaguliwa kidemokrasi, mpango wa kitengenezo wa aina nyingine ulianza kufanya kazi, ambao ulitambua mamlaka yenye kuweka rasmi yaliyo nje ya kutaniko la mahali na ambao ulitia mkazo mwingi zaidi katika kuhubiriwa kwa habari njema za Ufalme wa Mungu.g
-
-
Usitawi wa Muundo wa TengenezoMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
f Kupitia mwelekezi wa utumishi, utumishi wa shambani wa wale walioshirikiana na kutaniko, au darasa, ungeripotiwa kwa Sosaiti kila juma, kuanzia 1919.
g Kama ilivyoonyeshwa katika kijitabu Organization Method, kila kutaniko lilipaswa kuchagua mwelekezi-msaidizi na mweka-hazina. Hao, pamoja na mwelekezi aliyewekwa na Sosaiti walifanyiza halmashauri ya utumishi ya mahali.
-