Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kaeni Macho, Songeni Mbele kwa Ujasiri!
    Mnara wa Mlinzi—2002 | Aprili 1
    • Sehemu ya mwisho ya programu ilikuwa na mfululizo uliotolewa na washiriki watatu wa Baraza Linaloongoza. Mfululizo huo ulikuwa na kichwa “Huu Ndio Wakati wa Kukaa Macho, Kusimama Imara, na Kukua Katika Uweza.”—1 Wakorintho 16:13.

      Kwanza, Ndugu Stephen Lett alizungumzia kichwa “Kaeni Macho Wakati Huu wa Mwisho.” Ndugu Lett alieleza kwamba usingizi ni zawadi. Huo hutupatia nguvu. Hata hivyo, usingizi wa kiroho hauna faida yoyote. (1 Wathesalonike 5:6) Basi, tunawezaje kuendelea kuwa macho kiroho? Ndugu Lett alizungumzia “vidonge” vitatu vya kiroho: (1) Kuwa na mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana. (1 Wakorintho 15:58) (2) Ona uhitaji wako wa kiroho. (Mathayo 5:3) (3) Kubali shauri la Biblia ili utende kwa hekima.—Mithali 13:20.

      Ndugu Theodore Jaracz alitoa hotuba yenye kusisimua yenye kichwa “Simama Imara Chini ya Jaribu.” Akirejezea andiko la Ufunuo 3:10, Ndugu Jaracz aliuliza: “Ni nini ‘ile saa ya jaribu’?” Jaribu hilo linakuja “katika siku ya Bwana,” wakati huu tunamoishi. (Ufunuo 1:10) Jaribu hilo linahusu suala hili muhimu—je, tunatetea Ufalme wa Mungu unaotawala au tunatetea mfumo mwovu wa mambo wa Shetani? Kabla ya ile saa ya jaribu kumalizika, tutapatwa na majaribu au magumu. Je, tutabaki tukiwa waaminifu-washikamanifu kwa Yehova na tengenezo lake? ‘Ni lazima kila mmoja wetu aonyeshe uaminifu-mshikamanifu,’ akasema Ndugu Jaracz.

      Kwa kumalizia, Ndugu John E. Barr alitoa hotuba yenye kichwa “Kua Katika Uweza Ukiwa Mtu wa Kiroho.” Akirejezea andiko la Luka 13:23-25, alisema kwamba ni lazima tujikakamue ‘ili tuingie ndani kupitia mlango mwembamba.’ Wengi wanashindwa kwa sababu hawajitahidi kukua katika uweza. Ili tuwe Wakristo walio watu wazima, ni lazima tujifunze kutumia kanuni za Biblia katika kila sehemu ya maisha yetu. Ndugu Barr alihimiza hivi: “Nina hakika mtakubaliana nami kwamba huu ni wakati wa (1) kumtanguliza Yehova; (2) kukua katika uweza, na (3) kujikakamua kufanya mapenzi ya Yehova.” Kwa njia hiyo tutaweza kupitia mlango mwembamba unaoongoza kwenye maisha mazuri yasiyo na mwisho.”

  • Kaeni Macho, Songeni Mbele kwa Ujasiri!
    Mnara wa Mlinzi—2002 | Aprili 1
    • Hatimaye, wote walifurahi kumsikiliza Carey W. Barber mwenye umri wa miaka 96. Ndugu Barber alibatizwa mwaka wa 1921, naye amekuwa katika utumishi wa wakati wote kwa miaka 78. Ametumikia akiwa mshiriki wa Baraza Linaloongoza tangu mwaka wa 1978.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki