-
Kujulisha Habari Njema Bila Kuacha (1942-1975)Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Kuhusu mazoezi yake katika shule iliyoanzishwa kwenye Betheli ya Brooklyn katika 1942, George Gangas, mtafsiri Mgiriki wakati ule, alisema hivi baadaye: “Nakumbuka wakati nilipotoa hotuba yangu ya kwanza ya dakika sita. Sikujitumaini mwenyewe na hivyo nikaiandika. Lakini nilipoinuka kuitoa, nikakabwa na woga wa wasikilizaji nami niligugumia na kusema mashavuni, nikisahau niliyotaka kusema. Halafu nikaanza kusoma hati. Lakini mikono yangu ilikuwa ikitetemeka sana hivi kwamba mistari ilikuwa ikiruka juu-chini!” Hata hivyo, hakuacha. Baada ya wakati kupita akawa anatoa hotuba mbele ya wasikilizaji kwenye mikusanyiko mikubwa na hata kutumikia akiwa mshiriki wa Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova.
-
-
Kujulisha Habari Njema Bila Kuacha (1942-1975)Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
“Mtaala wa elimu ya Kikristo ya hali ya juu ulichukua majuma 20, Biblia ikiwa kitabu kikuu cha mafundisho,” aeleza Ndugu Schroeder, ambaye sasa hutumikia akiwa mshiriki wa Baraza Linaloongoza.
-