-
Sehemu ya 1—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya DuniaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Ndugu Russell alituma washirika wawili, J. C. Sunderlin na J. J. Bender, Uingereza ili kusimamia kazi ya kugawanya nakala 300,000 huko. Ndugu Sunderlin alienda London, hali Ndugu Bender alisafiri kwenda kaskazini katika Scotland na kisha akafanya kazi akielekea kusini. Majiji makubwa ndiyo yaliyokaziwa fikira zaidi. Kwa njia ya matangazo ya magazeti ya habari, watu wenye uwezo walipatikana, na mikataba ilifanywa pamoja nao wapate wasaidizi wa kutosha kugawanya mafungu yao ya nakala. Wagawanyaji karibu 500 waliajiriwa kazi katika London pekee. Kazi ilifanywa haraka, katika Jumapili mbili mfululizo.
-
-
Sehemu ya 1—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya DuniaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Ili kusaidia wale watu waliokuwa na njaa kiroho, baada ya safari ya Ndugu Russell katika 1891, jitihada zilizoongezwa zilifanywa kutafsiri fasihi katika lugha za Ulaya. Pia, mipango ilifanywa ili kuchapa na kuweka akiba ya fasihi katika London ili fasihi hizo ziweze kupatikana kwa urahisi kwa matumizi katika Uingereza. Shamba la Uingereza, lilithibitika kwelikweli kuwa tayari kuvunwa. Kufikia 1900, tayari kulikuwa makutaniko tisa na jumla ya Wanafunzi wa Biblia 138—miongoni mwao makolpota fulani wenye bidii. Wakati Ndugu Russell alipotembelea Uingereza tena katika 1903, watu elfu moja walikusanyika katika Glasgow ili kumsikia akihutubu juu ya “Matumaini na Matarajio ya Mileani,” 800 walihudhuria katika London, na wasikilizaji 500 kufikia 600 katika miji mingine.
-