Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kuhubiri na Kufundisha Duniani Kote
    2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Uingereza

      Reston, ambaye hakuwa amewahi kuanzisha funzo la Biblia kwa njia ya moja kwa moja, aliamua kujaribu njia hiyo. Kabla ya kubisha mlango wa kwanza, alisali kifupi, akimwomba Yehova amsaidie awe na maoni yanayofaa. Kisha akamweleza mwenye nyumba anayeitwa Andy mpango wa kujifunza Biblia. Andy alikubali mara moja kujifunza. Reston aliamua kumletea kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? baadaye siku hiyo. Alipokuwa akirudi huko kwa basi, Reston aligundua kwamba dereva wa basi hilo ni mtu aliyempelekea Mnara wa Mlinzi na Amkeni! kwa ukawaida. Kwa sababu alikuwa ametiwa moyo na jinsi Andy alivyoitikia asubuhi, aliamua kumwonyesha dereva mpango wetu wa kujifunza Biblia na watu bila malipo punde tu basi litakapofika mwisho wa safari.

      Wakati huohuo, abiria fulani mzee alitambua kwamba Reston ni Shahidi na akamwomba amtembelee rafiki yake mgonjwa ili amwombee. Reston alisema angefurahi kuzungumza naye na kumfariji kupitia Maandiko. Alitumia ile nakala aliyokuwa nayo ya kitabu Biblia Inafundisha, kumwonyesha abiria huyo jinsi funzo la Biblia linavyoweza kumsaidia. Mwanamke huyo alisema angependa funzo kama hilo. Kijana aliyekuwa ameketi upande ule mwingine alisikiliza mazungumzo yao. Alivutiwa na picha katika kitabu hicho. Hivyo kwa furaha Reston akaamua kumpa. Basi lilipofika mwisho wa safari, Reston alimweleza yule dereva kuhusu mpango wa kujifunza Biblia nyumbani bila malipo. Alishangaa dereva huyo alipokubali kwa shauku na kusema kwamba alikuwa na maswali mengi ya Biblia. Mara moja, Reston alienda kwa ndugu aliyeishi karibu ili kupata nakala nyingine ya kitabu Biblia Inafundisha na mwishowe akafika nyumbani kwa Andy jioni. Andy alichukua kitabu hicho kwa furaha. Alianza kujifunza Biblia na punde si punde akaanza kuishi kupatana na mambo aliyojifunza. Andy na yule dereva wa basi wanahudhuria mikutano, na Reston anaongoza mafunzo ya Biblia 15 ambayo aliyaanzisha kwa njia ya moja kwa moja. Sasa anahakikisha kwamba ana nakala kadhaa za kitabu Biblia Inafundisha anapohubiri.

      François na Monica pamoja na watoto wao wawili, walienda kwenye gari lao baada ya kuhubiri asubuhi. Hata hivyo, Shaé, binti yao mwenye umri wa miaka miwili na nusu hakutaka kuingia kwenye gari kabla ya kumpa mtu trakti yake ya mwisho. Wakati huo, gari fulani lilisimama upande ule mwingine wa barabara, na wanawake wawili wakashuka. Shaé alimpa mmoja wao trakti Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani, na Monica akamweleza trakti hiyo inazungumzia nini. Mwanamke huyo anayeitwa Sierra, alipendezwa na akamwalika Monica nyumbani kwake kujifunza Biblia pamoja na dada zake wenye umri wa chini ya miaka 20. Walipojifunza mara ya kwanza, Sierra aliuliza kama wana wake wawili wanaweza kujifunza Biblia. Baadaye, mwana wa dada ya Sierra alianza kujifunza pia. Mwishowe, hata Sierra alikubali kujifunza. Kisha mume wake akaanza kujifunza pia. Halafu mama ya Sierra, na vilevile watu wengine katika familia na marafiki, wakataka kujifunza Biblia. Azimio la Shaé la kupeana trakti yake ya mwisho lilifanya watu 11 waanze kujifunza Biblia. Wanne kati ya wanafunzi hao wanahudhuria mikutano ya kutaniko kwa ukawaida.

  • Kuhubiri na Kufundisha Duniani Kote
    2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • [Picha katika ukurasa wa 57]

      Reston akijifunza na Andy

      [Picha katika ukurasa wa 58]

      Shaé

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki