-
Umati Mkubwa Wenye Watu Wengi SanaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“Wao hawataona njaa tena wala kuona kiu tena, wala jua halitapiga juu yao tena wala joto lolote lenye kuunguza,
-
-
Umati Mkubwa Wenye Watu Wengi SanaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
27. (a) Isaya alitoaje unabii wa jambo linalofanana na maneno ya mzee? (b) Ni nini kinachoonyesha kwamba unabii wa Isaya ulianza kutimizwa juu ya kundi la Kikristo katika siku ya Paulo?
27 Acheni sisi tufikirie unabii ulio na maneno yanayofanana na hayo: “Hivi ndivyo Yehova amesema: ‘Katika wakati wa nia njema mimi nilijibu wewe, na katika siku ya wokovu mimi nimekusaidia wewe . . . Wao hawataenda njaa, wala hawataenda kiu, wala joto lenye kukausha au jua halitapiga wao. Kwa kuwa Mmoja ambaye ana sikitikio juu yao ataendesha wao, na kando ya chemchemi za maji yeye ataongoza wao.’” (Isaya 49:8, 10, NW; ona pia Zaburi 121:5, 6.) Mtume Paulo alinukuu sehemu ya unabii huu na akautumia kuhusu “siku ya wokovu” iliyoanza Pentekoste 33 W.K. Yeye aliandika: “Kwa maana yeye [Yehova] asema: ‘Katika wakati uliokubalika mimi nilisikia wewe, na katika siku ya wokovu mimi nilisaidia wewe.’ Tazama! Sasa ndio hasa wakati uliokubalika. Tazama! Sasa ndiyo siku ya wokovu.”—2 Wakorintho 6:2, NW.
28, 29. (a) Maneno ya Isaya yalitimizwaje katika karne ya kwanza? (b) Maneno ya Ufunuo 7:16 yanatimizwaje kwa habari ya umati mkubwa? (c) Ni nini litakalokuwa tokeo la kuelekezwa kwa umati mkubwa kwenye “vibubujiko vya maji ya uhai”? (d) Ni kwa nini umati mkubwa utakuwa usio na kifani miongoni mwa aina ya binadamu?
28 Ile ahadi ya kutoona njaa au kiu au kutaabishwa na joto lenye kukausha ilitumikaje wakati huo huko nyuma? Hakika, Wakristo katika karne ya kwanza walitaabishwa na njaa na kiu halisi nyakati nyingine. (2 Wakorintho 11:23-27) Ingawa hivyo, katika maana ya kiroho, wao walikuwa na chakula tele. Wao waliandaliwa kwa wingi hivi kwamba wao hawakwenda njaa au kiu kwa vitu vya kiroho. Zaidi ya hilo, Yehova hakuruhusu joto la kasirani yake liwake dhidi yao wakati yeye alipoharibu mfumo wa mambo wa Kiyahudi katika 70 W.K. Maneno ya Ufunuo 7:16 yana utimizo wa kiroho unaofanana na huo kwa ajili ya umati mkubwa leo. Pamoja na Wakristo wapakwa-mafuta, wao wanafurahia wingi wa maandalizi ya kiroho.—Isaya 65:13; Nahumu 1:6, 7.
29 Ikiwa wewe ni mmoja wa ule umati mkubwa, hali yako njema ya moyo itakufanya wewe “upige kilio kikuu kwa shangwe,” si kitu ulazimike kuvumilia nini kwa habari ya manyimo na mikazo wakati wa miaka hii ya gizagiza ya mfumo wa Shetani. (Isaya 65:14, NW) Katika maana hiyo, hata sasa, Yehova anaweza ‘kupangusa kabisa kila chozi kutoka macho yako.’ “Jua” lenye joto jingi la Mungu au hukumu mbaya halikutishi wewe tena, na pepo nne za uharibifu ziachiliwapo, huenda wewe ukakingwa na “joto lenye kuunguza” la kutopendezwa kwa Yehova.
-