-
Umati Mkubwa Wenye Watu Wengi SanaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Hiyo ndiyo sababu wao wako mbele ya kiti cha ufalme cha Mungu; na wao wanatolea yeye utumishi mtakatifu mchana na usiku katika hekalu lake; na Mmoja anayeketi juu ya kiti cha ufalme atatanda hema yake juu yao.’”—Ufunuo 7:14b, 15, NW.
-
-
Umati Mkubwa Wenye Watu Wengi SanaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
25. (a) Umati mkubwa unamtoleaje Yehova “utumishi mtakatifu mchana na usiku katika hekalu lake”? (b) Yehova ‘anatandaje hema lake’ juu ya umati mkubwa?
25 Na zaidi, wao wamekuwa Mashahidi wenye bidii wa Yehova—“wanatolea yeye utumishi mtakatifu mchana na usiku katika hekalu lake.” Je! wewe ni mmoja wa huu umati mkubwa ulio wakfu? Ikiwa ndivyo, ni pendeleo lako kutumikia Yehova bila kuacha katika ua wake wa kidunia wa hekalu lake kubwa la kiroho. Leo, chini ya mwelekezo wa wapakwa-mafuta, umati mkubwa unafanya sehemu iliyo kubwa zaidi ya kazi ya kutoa ushuhuda. Wajapokuwa na madaraka ya kimwili, mamia ya maelfu wanautafutia nafasi ule utumishi wa wakati wote wakiwa mapainia. Lakini uwe wewe ni wa kikundi hicho au la, ukiwa mshiriki aliye wakfu wa umati mkubwa, wewe unaweza kushangilia ukiwa rafiki ya Mungu na mgeni anayekaribishwa katika hema yake. (Zaburi 15:1-5; Yakobo 2:21-26)
-