-
Sehemu ya 2—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya DuniaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Katikati ya mkazo huo uliokuwa ukiongezeka, katika 1935, Mashahidi wa Yehova walipata uelewevu ulio wazi kutoka katika Biblia wa utambulisho wa ile “halaiki kubwa,” au “umati mkubwa,” wa Ufunuo 7:9-17. (KJ, NW) Uelewevu huo uliwawezesha kupata kujua juu ya kazi ya haraka na isiyotazamiwa. (Isa. 55:5) Hawakuwa tena na maoni ya kwamba wote ambao si wa “kundi dogo” la warithi wa Ufalme wa kimbingu wangepata fursa wakati fulani ujao ya kupatanisha maisha zao na matakwa ya Yehova. (Luka 12:32) Walitambua kwamba wakati ulikuwa umefika wa kufanya wanafunzi wa watu hao sasa ili wapate kuokolewa kuingia katika ulimwengu mpya wa Mungu. Hawakujua kukusanywa kwa huo umati mkubwa kutoka mataifa yote kungeendelea kwa muda mrefu kadiri gani, ingawa walihisi kwamba mwisho wa mfumo mwovu wa mambo lazima uwe ulikuwa karibu sana. Hawakuwa na hakika kazi hiyo ingetimizwaje kwa sababu ya kuelekeana na mnyanyaso uliokuwa ukienea na kuzidi kuwa wenye ukatili. Hata hivyo, walikuwa na uhakika kwamba—kwa kuwa ‘mkono wa Yehova si mfupi mno,’ yeye angewafungulia njia ili watimize mapenzi yake.—Isa. 59:1.
-
-
Sehemu ya 3—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya DuniaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Mwaka 1935 ni wa maana sana kwa sababu wakati huo ile halaiki kubwa, au umati mkubwa, wa Ufunuo 7:9 ulipata kutambulishwa. Kuhusiana na kukusanywa kwa kikundi hicho, Mashahidi wa Yehova walianza kutambua kwamba Biblia iliweka mbele yao kazi ya kadiri kubwa zaidi ya yoyote iliyoitangulia.
-