-
Imani Yako Katika Ufufuo Ni Yenye Nguvu Kadiri Gani?Mnara wa Mlinzi—1998 | Julai 1
-
-
12. Jumuiya ya Wakristo ilipata wapi fundisho lake kuhusu nafsi isiyoweza kufa?
12 Kwa nini Jumuiya ya Wakristo hufundisha mambo tofauti na yale Biblia husema? Kichapo New Catholic Encyclopedia, katika makala yake ya “Kutoweza Kufa kwa Nafsi na kwa Binadamu,” chasema kwamba Waandishi wa Kanisa walitegemeza imani yao juu ya nafsi isiyoweza kufa, katika “washairi na wanafalsafa na dhana ya kimapokeo ya Kigiriki wala si katika Biblia . . . Baadaye, wasomi walipendelea kutumia imani ya Plato au kanuni za Aristotle.” Kichapo hicho chataarifu kwamba “uvutano wa dhana ya Uplato na Uplato mpya”—kutia na imani katika nafsi isiyoweza kufa—hatimaye ziliingizwa “katika mambo ya msingi ya theolojia ya Kikristo.”
-
-
Imani Yako Katika Ufufuo Ni Yenye Nguvu Kadiri Gani?Mnara wa Mlinzi—1998 | Julai 1
-
-
Mwili na Nafsi
18. Wanafalsafa fulani Wagiriki waliitikiaje taarifa ya Paulo ya kwamba Yesu alikuwa amefufuliwa, na kwa nini?
18 Alipokuwa Athene, mtume Paulo alihubiri habari njema kwa umati uliotia ndani wanafalsafa Wagiriki. Walisikiliza mazungumzo hayo kuhusu Mungu mmoja wa kweli na mwito wake wa toba. Lakini ni nini kilichotukia baadaye? Paulo alimalizia hotuba yake kwa kusema hivi: “[Mungu] ameweka siku ambayo katika hiyo akusudia kuihukumu kwa uadilifu dunia inayokaliwa kwa njia ya mwanamume ambaye ameweka rasmi, naye ametoa uhakikisho kamili kwa watu wote kwa kuwa amemfufua kutoka kwa wafu.” Maneno hayo yalitokeza mvurugo. “Waliposikia juu ya ufufuo wa wafu, wengine wao wakaanza kudhihaki.” (Matendo 17:22-32) Mwanatheolojia Oscar Cullmann asema hivi: “Kwa Wagiriki walioamini kwamba nafsi haiwezi kufa, huenda lilikuwa jambo gumu zaidi kwao kukubali yale Wakristo waliyohubiri kuhusu ufufuo kuliko ilivyokuwa kwa wengine. . . . Fundisho la Socrates na Plato, waliokuwa wanafalsafa wakuu, haliwezi kwa vyovyote kupatanishwa [kukubaliana] na fundisho la Agano Jipya.”
-