-
Kutafuta Mambo Yaliyokusudiwa Kimbele ya MwanadamuAmkeni!—1999 | Agosti 8
-
-
Ugiriki na Roma
Inapohusu mambo ya kidini, “Ugiriki ya kale haikukosa kuathiriwa na uvutano mkubwa wa Babilonia,” asema Jean Bottéro. Profesa Peter Green aeleza kwa nini itikadi ya tukio lililopangwa lisiloepukika ilipendwa na wengi katika Ugiriki: “Katika ulimwengu usiotumainika, ambamo watu walihofia sana matokeo ya maamuzi yao wenyewe, na mara nyingi wakajihisi wakiwa watumwa tu, wakielekezwa huku na huku na uhitaji wa kufuata yaliyoamuliwa maishani mwao ambayo yalikuwa ya kifumbo na yasiyobadilika, amri ya miungu ilikuwa njia mojawapo ambayo wakati ujao wa mtu uliweza kupangwa. Mambo yaliyoamuliwa kimbele yangeweza kutabiriwa kwa kutumia ujuzi wa pekee au maono. Huenda ikawa habari asiyopenda kusikia; lakini angalau akiwa ameonywa kimbele angeweza kujitayarisha.”
Mbali na kuwahakikishia watu juu ya wakati ujao, kuitikadi kwamba maisha yameamuliwa kimbele kulitumiwa pia kwa makusudi mengine mabaya. Wazo la kuamuliwa kimbele kwa maisha lilisaidia kutiisha umma, na kwa sababu hiyo, kulingana na mwanahistoria F. H. Sandbach, “itikadi ya kwamba ulimwengu mzima ulitawalwa na Uongozi wa Kimungu ungewavutia jamii ya watawala.”
Kwa nini? Profesa Green aeleza kwamba itikadi hii “ilitetea haki ya—kiadili, kitheolojia, na umaana—wa mfumo wa kijamii na wa kisiasa: ilikuwa mbinu yenye uwezo na hila ya kujifaidi iliyowahi kubuniwa na watawala wa Ugiriki. Uhakika wa kwamba jambo lolote laweza kutukia ulimaanisha kwamba ilikuwa imeamuliwa litukie; na kwa kuwa maumbile yalikuwa na mwelekeo unaofaa kwa wanadamu, jambo lililoamuliwa ni lazima liwe lilifaa.” Kwa kweli, lilitokeza “uteteaji wa haki za kibinafsi zenye ukatili.”
Jambo la kwamba wengi waliamini maisha yameamuliwa kimbele linadhihirishwa na fasihi za Kigiriki. Baadhi ya mitindo ya fasihi za kale iliyokuwapo ni mashairi marefu, hekaya, na tanzia—iliyokazia sana kuamuliwa kimbele kwa maisha. Kulingana na ngano za Kigiriki, mwisho wa mwanadamu uliwakilishwa na miungu ya kike mitatu iliyoitwa Moirai. Klotho alisokota uzi wa uhai, Lakesisi aliamua urefu wa maisha, na Atropo aliukata muda wa uhai ulipokwisha.
-
-
Kutafuta Mambo Yaliyokusudiwa Kimbele ya MwanadamuAmkeni!—1999 | Agosti 8
-
-
Waroma na Wagiriki walikuwa na hamu ya kujua tukio lisiloepukika ambalo lilidhaniwa kuwa lingewapata mwishowe. Hivyo, waliiga na kuendeleza zaidi unajimu na uaguzi wa Babiloni.
-
-
Kutafuta Mambo Yaliyokusudiwa Kimbele ya MwanadamuAmkeni!—1999 | Agosti 8
-
-
Kufikia karne ya tatu K.W.K., unajimu ulipendwa sana katika Ugiriki, na katika mwaka wa 62 K.W.K., buruji ya kale zaidi ya mambo ya nyota ya Wagiriki ikabuniwa. Wagiriki walipendezwa sana na unajimu hivi kwamba kulingana Profesa Gilbert Murray, unajimu “uliathiri sana fikira za Wagiriki jinsi ambavyo ugonjwa mpya unavyozukia watu wanaoishi katika kisiwa cha mbali.”
Katika kujaribu kujua matukio ya wakati ujao, Wagiriki na Waroma walienda sana kwa waaguzi au wawasiliani-roho. Ilidhaniwa kwamba miungu iliwasiliana na wanadamu kupitia watu. (Linganisha Matendo 16:16-19.) Matokeo ya itikadi hizi yalikuwa nini? Mwanafalsafa Bertrand Russell alisema hivi: “Hofu ikazuka badala ya tumaini; kusudi la maisha lilikuwa kuepuka misiba badala ya kutumia maisha kwa njia inayofaa.” Mambo kama hayo yakawa ubishi katika Jumuiya ya Wakristo.
-