-
Je, Unafuata “Njia Iliyo Bora Zaidi” Ya Upendo?Mnara wa Mlinzi—2009 | Julai 15
-
-
Kati ya maneno hayo, neno a·gaʹpe ndilo neno linalotumiwa kueleza kuhusu Mungu ambaye “ni upendo.”a Kuhusu upendo huo, Profesa William Barclay anasema hivi katika kitabu chake (New Testament Words): “Upendo wa Agapē unahusiana na akili: si hisia tu inayojitokeza yenyewe katika mioyo yetu; ni kanuni ambayo tunachagua kuishi kupatana nayo bila kulazimishwa. Upendo wa Agapē unategemea hasa hiari” au kupenda. Katika hali hii, a·gaʹpe ni upendo unaoongozwa na kanuni, lakini mara nyingi unaambatana na hisia zenye nguvu. Kwa kuwa kuna kanuni nzuri na mbaya, ni wazi kwamba Wakristo wanapaswa kuongozwa na kanuni nzuri ambazo Yehova Mungu mwenyewe ameweka katika Biblia. Tunapolinganisha maelezo ya Biblia kuhusu a·gaʹpe na maneno mengine yanayotumiwa katika Biblia kuelezea upendo, tutaelewa vizuri zaidi upendo ambao tunapaswa kuonyesha.
-
-
Je, Unafuata “Njia Iliyo Bora Zaidi” Ya Upendo?Mnara wa Mlinzi—2009 | Julai 15
-
-
Si kosa kuwa na rafiki wa karibu katika kutaniko. Hata hivyo, katika 2 Petro 1:7, tunatiwa moyo tuongeze upendo (a·gaʹpe) kwenye ‘upendo wetu wa kindugu’ (phi·la·del·phiʹa, neno linalotokana na maneno mawili, phiʹlos, neno la Kigiriki linalotafsiriwa “rafiki,” na a·del·phosʹ, neno la Kigiriki linalotafsiriwa “ndugu”). Ili kufurahia urafiki wa kudumu, tunahitaji kutumia shauri hilo. Tunapaswa kujiuliza hivi: ‘Je, hisia zangu za urafiki zinasawazishwa na kanuni za Biblia?’
Neno la Mungu linatusaidia kuepuka kuonyesha ubaguzi tunaposhughulika na marafiki wetu. Hatupaswi kutumia viwango viwili tofauti: kiwango kisicho na masharti magumu kwa ajili ya marafiki wetu na kiwango tofauti, chenye masharti magumu kwa ajili ya watu ambao si marafiki wetu. Zaidi ya hayo, hatupaswi kuwasifu-sifu watu au kuwapaka mafuta ili wawe marafiki wetu. Jambo la maana zaidi ni kwamba tunapotumia kanuni za Biblia tunakuwa na utambuzi unaohitajiwa katika kuchagua marafiki na kuepuka ‘mashirika mabaya ambayo yanaharibu tabia nzuri.’—1 Kor. 15:33.
-
-
Je, Unafuata “Njia Iliyo Bora Zaidi” Ya Upendo?Mnara wa Mlinzi—2009 | Julai 15
-
-
Upendo wa familia unahusiana na moyo wetu na hisia zetu. Hata hivyo, inapendeza kujua kwamba Paulo alitumia neno a·gaʹpe kueleza kuhusu upendo ambao mume anapaswa kumwonyesha mke wake. Paulo alilinganisha upendo huo na upendo ambao Kristo analionyesha kutaniko. (Efe. 5:28, 29) Upendo huo unategemea kanuni zilizowekwa na Yehova, Mwanzilishi wa mpango wa familia.
Upendo wa kweli kwa washiriki wa familia unatuchochea kupendezwa na wazazi wetu waliozeeka au unatuchochea kutimiza daraka la kuwatunza watoto wetu. Unawachochea pia wazazi kuwatia nidhamu watoto wao kwa upendo inapohitajika na unawazuia wazazi kutenda tu kwa hisia, jambo ambalo mara nyingi linawafanya wazazi wawaache watoto wafanye jambo lolote wanalotaka.—Efe. 6:1-4.
-
-
Je, Unafuata “Njia Iliyo Bora Zaidi” Ya Upendo?Mnara wa Mlinzi—2009 | Julai 15
-
-
Mtume Paulo aliandika hivi: “Upendo wenu na uwe bila unafiki. . . . Katika upendo wa kindugu iweni na upendo mwororo kwa mtu na mwenzake.” (Rom. 12:9, 10) Kwa kweli, Wakristo wana ‘upendo (a·gaʹpe) bila unafiki.’ Upendo huo hautegemei tu hisia inayojitokeza katika mioyo yetu. Badala yake, unategemea kabisa kanuni za Biblia.
-
-
Je, Unafuata “Njia Iliyo Bora Zaidi” Ya Upendo?Mnara wa Mlinzi—2009 | Julai 15
-
-
a Neno a·gaʹpe linatumiwa pia kuhusiana na matendo yasiyofaa.—Yoh. 3:19; 12:43; 2 Tim. 4:10; 1 Yoh. 2:15-17.
-