Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ukweli Kuhusu Ekaristi
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Aprili 1
    • “Huu Unamaanisha” Ama “Huu Ndio”?

      Kwa kweli, Biblia fulani zinatafsiri hivi maneno ya Yesu: “Twaeni, mle; huu ndio mwili wangu,” na, “Nyweni nyote katika hiki; kwa maana hii ndiyo damu yangu.” (Mathayo 26:26-28, Union Version) Pia, ni kweli kwamba neno la Kigiriki e·stin΄, ambalo ni namna ya kitenzi cha Kigiriki “kuwa,” linamaanisha “ndio.” Lakini kitenzi hichohicho kinaweza kumaanisha “kuwakilisha.” Inapendeza kwamba katika Biblia nyingi, mara nyingi kitenzi hicho kinatafsiriwa “maana ya” au “mfano wa.”b Muktadha ndio unaoamua jinsi kitenzi hicho kitakavyotafsiriwa. Kwa mfano katika Biblia nyingi, neno e·stin΄ katika Mathayo 12:7 linatafsiriwa kuwa “maanisha.” Andiko hilo linasema hivi: “Kama mngalijua maana yake [Kigiriki, e·stin΄] maneno haya, nataka rehema, wala si sadaka, msingaliwalaumu wasio na hatia.”—UV; Zaire Swahili Bible.

      Kwa sababu hiyo, wasomi wengi wa Biblia wanaoheshimiwa wamekubaliana kwamba neno “ndio” halitoi maana sahihi ya wazo la Yesu. Kwa mfano, Jacques Dupont alifikiria utamaduni na jamii ambamo Yesu aliishi na akakata kauli kwamba “njia ya kawaida zaidi” ya kutafsiri mstari huo inapaswa kuwa: “Huu unamaanisha mwili wangu.”

  • Ukweli Kuhusu Ekaristi
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Aprili 1
    • b Kwa mfano, ona maandiko ya Mathayo 27:46; Luka 8:11; Wagalatia 4:24 kama yalivyotafsiriwa katika UV, ZSB, na Biblia Habari Njema.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki