Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jitihada za Kutafsiri Biblia Katika Kigiriki cha Kisasa
    Mnara wa Mlinzi—2002 | Novemba 15
    • Mtafsiri Jasiri

      Licha ya upinzani mkali, watu walikuwa na hamu kubwa ya kujifunza Biblia. Hivyo mtu mmoja mashuhuri alijitokeza kufanya kazi muhimu ya kutafsiri Biblia katika Kigiriki cha kisasa. Mtu huyo jasiri alikuwa Neofitos Vamvas, mtaalamu wa lugha na msomi maarufu wa Biblia, ambaye alionwa na wengi kuwa miongoni mwa “Walimu wa Taifa.”

      Vamvas aliamini kwamba Kanisa Othodoksi ndilo lililowatumbukiza watu katika giza la kiroho. Aliamini kabisa kwamba Biblia ilihitaji kutafsiriwa katika Kigiriki cha kawaida ili kuwaamsha watu kiroho. Mnamo mwaka wa 1831, yeye pamoja na wasomi wengine, walianza kutafsiri Biblia kwa Kigiriki cha wasomi. Tafsiri yake nzima ilichapishwa mwaka wa 1850. Alishirikiana na Chama cha Biblia cha Uingereza na cha Lugha za Kigeni (BFBS) katika kuchapisha na kugawanya tafsiri yake kwa kuwa Kanisa Othodoksi la Ugiriki lilikataa kumsaidia. Kanisa lilimwita “Mprotestanti,” na baada ya muda alitengwa na kanisa.

      Tafsiri ya Vamvas ilitegemea kabisa tafsiri ya King James Version na hivyo ilikuwa na kasoro kama tafsiri hiyo kwa sababu wakati huo watu hawakujua vyema lugha wala kazi ya kutafsiri Biblia. Hata hivyo, kwa miaka mingi, hiyo ndiyo iliyokuwa Biblia pekee iliyotafsiriwa katika Kigiriki cha kisasa. Jambo la kuvutia ni kwamba jina la Mungu likiwa limeandikwa “Ieová” linapatikana mara nne ndani ya tafsiri hiyo.—Mwanzo 22:14; Kutoka 6:3; 17:15; Waamuzi 6:24.

      Watu walikuwa na maoni gani kuhusu Biblia hii na Biblia nyingine zilizotafsiriwa kwa lugha rahisi? Walisisimuka ajabu! Kwenye mashua iliyokuwa karibu na ufuo wa kisiwa kimoja cha Ugiriki, muuzaji mmoja wa Biblia wa chama cha BFBS “alizingirwa na mashua zilizojaa watoto waliotaka [Biblia], hivi kwamba alilazimika . . . kumwagiza nahodha afunge safari” la sivyo, angegawa nakala zote alizokuwa nazo mahali hapo. Lakini wapinzani walichukua hatua mara moja.

      Makasisi Waothodoksi waliwaonya watu wasichukue tafsiri hizo. Kwa mfano, katika jiji la Athens, Biblia zote zilikusanywa kwa nguvu. Katika mwaka wa 1833, askofu Mwothodoksi wa Crete aliteketeza Biblia za “Agano Jipya” alizopata kwenye nyumba moja ya watawa. Kasisi mmoja na wakazi wa vijiji vya karibu walificha nakala zao hadi askofu huyo alipoondoka kisiwani.

      Miaka kadhaa baadaye, kwenye kisiwa cha Corfu, tafsiri ya Biblia ya Vamvas ilipigwa marufuku na Sinodi Takatifu ya Kanisa Othodoksi la Ugiriki. Uuzaji wa Biblia hiyo ulipigwa marufuku, na nakala zilizosalia zikaharibiwa. Biblia ziliteketezwa kwenye visiwa vya Chios, Síros, na Mykonos kwa sababu ya upinzani wa makasisi.

  • Jitihada za Kutafsiri Biblia Katika Kigiriki cha Kisasa
    Mnara wa Mlinzi—2002 | Novemba 15
    • Kwa sasa, Mashahidi wa Yehova wanaongoza katika kazi ya kuwafundisha watu Biblia nchini Ugiriki kama wanavyofanya katika nchi nyingine nyingi. Tangu mwaka wa 1905, wametumia tafsiri ya Vamvas kufundisha maelfu ya watu wanaozungumza Kigiriki kuhusu ujuzi juu ya kweli ya Biblia.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki