-
Yehova Anasikiliza Kilio cha Mtu wa Hali ya ChiniMnara wa Mlinzi—2010 | Novemba 15
-
-
Fikiria kisa cha mzee Mkristo anayeitwa Alex, ambaye alikuwa ameoa karibuni lakini mke wake akafa kwa ghafula kutokana na ugonjwa usioweza kutibiwa. Mwangalizi mmoja anayesafiri mwenye huruma alichukua hatua ya kumwambia Alex maneno yanayofariji. Yeye pia alikuwa amefiwa na mke wake lakini alioa mke mwingine. Mwangalizi huyo anayesafiri alieleza jinsi alivyolemewa sana na hisia. Alijisikia vizuri alipokuwa na wengine katika huduma na katika mikutano ya kutaniko. Hata hivyo, aliporudi katika chumba chake na kufunga mlango alijisikia mpweke sana. Alex anasema hivi: “Nilipata faraja kama nini kujua kwamba hisia ambazo nilikuwa nazo zilikuwa za kawaida na wengine wamewahi kuhisi hivyo.” Bila shaka, “neno linalosemwa wakati unaofaa” linaweza kumfariji mtu na kumtegemeza wakati wa taabu.—Met. 15:23.
Mzee mwingine Mkristo, ambaye anawafahamu watu wengi ambao walifiwa na wenzi wao wa ndoa, alichochewa kuzungumza na Alex maneno machache yenye kutia moyo. Akiwa na hisia-mwenzi, alimwambia kwa upendo kwamba Yehova anajua jinsi tunavyohisi na tunachohitaji. Ndugu huyo alisema hivi: “Ikiwa katika miezi na miaka inayokuja, utahisi kwamba unahitaji mwenzi wa ndoa, kwa upendo Yehova ameweka sasa uandalizi wa kuoa au kuolewa tena.” Bila shaka, si kila mtu aliyefiwa na mwenzi wa ndoa na ambaye anatamani kuoa au kuolewa tena anayeweza kufanya hivyo. Lakini alipotafakari kuhusu maneno ya ndugu huyo, Alex alisema hivi: “Kukumbushwa kwamba huo ni uandalizi wa Yehova kunaondoa mawazo yoyote yasiyofaa ya kwamba kuoa au kuolewa tena wakati ujao ni kukosa ushikamanifu kwa mwenzi wako wa ndoa aliyekufa au kwa mpango wa ndoa wa Yehova.”—1 Kor. 7:8, 9, 39.
-
-
Yehova Anasikiliza Kilio cha Mtu wa Hali ya ChiniMnara wa Mlinzi—2010 | Novemba 15
-
-
Alex alikubali hivi: “Mwenzi wako wa ndoa anapokufa, mawazo yasiyofaa yanajaa katika akili yako.” Anakumbuka kwamba alijiuliza hivi: “‘Je, kuna jambo lolote ambalo ningefanya kwa njia tofauti? Je, ningeweza kuwa mwenye ufikirio zaidi na mwenye kujali zaidi?’ Sikutaka kuwa peke yangu. Sikutaka kuwa mjane. Ni vigumu sana kuacha mawazo hayo kwa sababu kila siku unakumbushwa kwamba uko peke yako.”
-
-
Yehova Anasikiliza Kilio cha Mtu wa Hali ya ChiniMnara wa Mlinzi—2010 | Novemba 15
-
-
Alex anasema hivi kutokana na mambo aliyojionea mwenyewe: “Tukitimiza sehemu yetu kwa kutumia maandalizi yote ambayo Yehova Mungu anatupatia ili kutusaidia kuwa wenye nguvu kiroho, tutakuwa na ‘nguvu zinazopita zile za kawaida’ za kutuwezesha kuvumilia jaribu lolote ambalo huenda tukakabili.”—2 Kor. 4:7.
-