-
Naweza Kuishije Nikiwa na Huzuni Yangu?Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa
-
-
“NILIHISI kusongwa sana nizuie hisia zangu,” aeleza Mike alipokumbuka kifo cha baba yake. Kwa Mike, kuzuia huzuni yake lilikuwa jambo la kiume kufanya. Hata hivyo baadaye aling’amua kwamba alikuwa amekosea. Kwa hiyo rafikiye Mike alipofiwa na babu yake, Mike alijua jambo la kufanya. Yeye asema hivi: “Miaka michache iliyopita, ningalimpigapiga begani na kusema ‘Uwe mwanamume.’ Sasa niligusa mkono wake na kusema, ‘Hisi vile utakavyo kuhisi. Hilo litakusaidia ushughulike vya kufaa na hali hii. Ikiwa wataka niende, nitaenda. Ikiwa wataka nikae, nitakaa. Lakini usiogope kuhisi.’”
-
-
Naweza Kuishije Nikiwa na Huzuni Yangu?Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa
-
-
Mwanamke mmoja mchanga aeleza jinsi rafiki wa karibu alivyomsaidia ashughulike vya kufaa na hali wakati mama yake alipokufa. Yeye akumbuka hivi: “Sikuzote rafiki yangu alikuwapo kwa ajili yangu. Alilia pamoja nami. Aliongea nami. Niliweza tu kuonyesha hisiamoyo zangu waziwazi sana, na hilo lilikuwa jambo la maana kwangu. Sikuhitaji kuaibika kwa sababu ya kulia.” (Ona Warumi 12:15.)
-