Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je! Ni Kawaida Kuhisi Hivi?
    Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa
    • Unapofiwa na Mwenzi wa Ndoa

      Kufiwa na mwenzi wa ndoa ni aina nyingine ya umivu kali la kimoyoni, hasa ikiwa wote wawili waliishi maisha yenye utendaji mwingi wakiwa pamoja. Hilo laweza kumaanisha mwisho wa mtindo-maisha mzima walioshiriki pamoja, mwisho wa kusafiri, wa kufanya kazi, wa kuwa na vitumbuizo, na wa kutegemeana.

      Eunice aeleza yale yaliyotendeka wakati mume wake alipokufa ghafula kutokana na ugonjwa wa moyo. “Kwa juma la kwanza, nilikuwa katika hali ya kutohisi lolote kihisiamoyo, kana kwamba mwili wangu haukuwa ukifanya kazi tena. Hata sikuweza kuonja wala kunusa. Hata hivyo, hisi yangu ya kufikiri vizuri iliendelea ikiwa imejitenga. Kwa sababu nilikuwa nimekuwa na mume wangu walipokuwa wakijaribu kusawazisha hali yake kwa kutumia CPR (utaratibu wa kumhuisha mtu ili aanze kupumua kikawaida) pamoja na madawa, sikupatwa na zile dalili za kawaida za kukana. Hata hivyo, nilihisi kukata tamaa sana, kana kwamba nilikuwa nikitazama gari likianguka kutoka gengeni (mteremko wa ghafula) nami singeweza kufanya lolote juu yalo.”

      Je! alitoa machozi? “Bila shaka nilifanya hivyo, hasa niliposoma yale mamia ya kadi za kusikitikia nilizokuwa nimepokea. Nililia kwa kila moja. Hilo lilinisaidia kujiweza hadi sehemu iliyobaki ya siku. Lakini hakuna chochote ambacho kingeweza kusaidia nilipoulizwa mara kwa mara jinsi nilivyohisi. Bila shaka, nilikuwa katika hali ya kuhuzunika sana.”

      Ni nini kilichomsaidia Eunice avumilie huzuni yake? “Bila kung’amua, niliamua kuendelea na maisha yangu bila kujua,” yeye asema. “Hata hivyo, jambo liniumizalo bado ni wakati nikumbukapo kwamba mume wangu, aliyependa uhai sana, hayupo hapa kuufurahia.”

  • Naweza Kuishije Nikiwa na Huzuni Yangu?
    Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa
    • MaryAnne pia alihisi kusongwa azuie hisia zake wakati mume wake alipokufa. “Nilihangaikia sana kuwekea wengine kielelezo chema,” yeye akumbuka, “hivi kwamba sikujiruhusu nionyeshe hisia za kawaida. Lakini hatimaye nilijifunza kwamba kujaribu kuwa nguzo ya imara kwa ajili ya wengine hakukuwa kunanisaidia. Nilianza kuchanganua hali yangu na kusema, ‘Lia ikiwa ni lazima ulie. Usijaribu kuwa imara mno. Onyesha hisia zako zote kabisa.’”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki