-
Kukabiliana na Hisia Mpendwa AnapokufaAmkeni!—2011 | Aprili
-
-
Kukabiliana na Hisia Mpendwa Anapokufa
“Nilishtuka na kuwa hoi nilipopata habari za kifo cha baba yangu. Nililemewa na hisia za hatia kwa kuwa sikuwa karibu alipokufa. Hakuna kitu kinachoweza kulinganishwa na uchungu mwingi sana ambao mtu huhisi anapofiwa na mpendwa wake. Ninamkosa sana baba yangu!”—Sara.
-
-
Kukabiliana na Hisia Mpendwa AnapokufaAmkeni!—2011 | Aprili
-
-
“Sikupata Nafasi ya Kuomboleza”
Fikiria kisa cha Nathaniel, mwanamume ambaye alifiwa na mama yake alipokuwa na umri wa miaka 24. Anasema: “Kwanza nilichanganyikiwa. Nilihisi kwamba ninapaswa kumfariji baba yangu na marafiki wengi wa mama ambao walikuwa na huzuni. Sikupata nafasi ya kuomboleza.”
Baada ya zaidi ya mwaka mmoja, Nathaniel aligundua kwamba bado hakuwa amekabiliana na hisia za kifo cha mama yake. Anasema: “Bado Baba hunipigia simu mara kwa mara kunieleza hisia zake, na ni vizuri kwamba anafanya hivyo. Anahitaji kuzungumza kuhusu hisia zake, nami ninafurahi kumsaidia. Lakini mimi ninapohitaji faraja, ninahisi kwamba sina yeyote wa kunifariji.”
-
-
Kukabiliana na Hisia Mpendwa AnapokufaAmkeni!—2011 | Aprili
-
-
“Nilijihisi Nikiwa Mpweke Bila Mama”
Huenda upweke ndilo tatizo kubwa zaidi ambalo huwapata wale ambao wamefiwa na mpendwa wao. Kwa mfano, Ashley alikuwa na umri wa miaka 19 mama yake alipokufa kutokana na kansa. Anasema: “Baadaye nilijihisi nikiwa nimechanganyikiwa kabisa na mpweke sana. Mama alikuwa ndiye rafiki yangu wa karibu zaidi. Tulikuwa pamoja mara nyingi!”
Inaeleweka kwamba Ashley aliona ugumu wa kurudi nyumbani kila siku na kutambua kwamba mama yake hayupo. Anasema: “Nilijihisi nikiwa mpweke bila mama. Mara nyingi nilienda chumbani na kulia huku nikitazama picha zake na kufikiria kuhusu mambo ambayo tulikuwa tukifanya pamoja.”
-