Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ninaweza Kudhibiti Jinsi Gani Hisia Zangu?
    Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2
    • Kuvumilia Huzuni

      “Hivi majuzi nimekuwa nikijiona sifai kitu, tena sina furaha,” asema Laura, mwenye umri wa miaka 16. “Sifurahii maisha hata kidogo. Mimi hulia sana kitandani.” Kama Laura, vijana wengi huhisi kwamba wanalemewa na ugumu wa maisha. Namna gani wewe? Mikazo mingi sana kutoka kwa wazazi wako, marafiki, walimu; mabadiliko ya kimwili na kihisia ya wakati wa kubalehe; au kuhisi kwamba hufai kitu kwa sababu ya kosa fulani dogo—yote hayo yanaweza kukufanya ujisikie vibaya sana.

      Vijana fulani hata huanza kujiumiza ili kupunguza huzuni hiyo.b Ikiwa umetumbukia katika zoea hilo, jaribu kujua ni kwa nini. Kwa mfano, mara nyingi watu ambao hujiumiza, hufanya hivyo wanapokuwa na mkazo. Je, kuna hali fulani—labda inayohusisha familia au marafiki—inayokufanya uwe na mkazo?

      Njia moja nzuri ya kushughulika na hisia zinazosumbua ni kuzungumza na mzazi au mshiriki mkomavu wa kutaniko anayeweza kuwa ndugu “aliyezaliwa kwa ajili ya wakati wa taabu.” (Methali 17:17) Liliana, mwenye umri wa miaka 16, alizungumza na akina dada fulani wakomavu. “Kwa kuwa wana umri mkubwa kuliko wangu,” anasema, “wana mashauri mazuri. Wamekuja kuwa rafiki zangu.”c Dana, mwenye umri wa miaka 15, anasema kwamba alipata nafuu kwa kushiriki zaidi katika huduma ya Kikristo. “Hilo ndilo jambo bora ambalo ningeweza kufanya,” anasema. “Huo ndio wakati nilipokuwa na furaha zaidi maishani!”

      Zaidi ya yote, ikiwa una huzuni au umeshuka moyo, usipuuze sala. Mtunga-zaburi Daudi, aliyekumbwa na taabu nyingi, aliandika: “Mtupie Yehova mzigo wako, naye mwenyewe atakutegemeza.” (Zaburi 55:22) Yehova anajua jinsi unavyoteseka. Isitoshe, ‘anakujali.’ (1 Petro 5:7) Ikiwa moyo wako unakulaumu, kumbuka kwamba ‘Mungu ni mkuu kuliko moyo wako naye anajua mambo yote.’ (1 Yohana 3:20) Anaelewa vizuri zaidi kuliko wewe ni kwa nini unafadhaika, naye anaweza kukuondolea mzigo wa kihisia unaokulemea.

      Huzuni ikiendelea, inawezekana kwamba una tatizo fulani la afya, kama vile ugonjwa wa kushuka moyo.d Ikiwa hivyo ndivyo ilivyo, ingefaa umwone daktari. Kupuuza hali hiyo ni kama kuongeza sauti ya redio katika gari ili usisikie makelele yanayotoka katika injini ya gari. Ingefaa zaidi ushughulikie hali hiyo. Kwa kweli, hakuna haja ya kuonea aibu hali yako. Vijana wengi walio na ugonjwa wa kushuka moyo au matatizo mengine kama hayo wanapata msaada kupitia matibabu.

  • Ninaweza Kudhibiti Jinsi Gani Hisia Zangu?
    Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2
    • b Watu wanaojiumiza hufanya hivyo kimakusudi kwa njia mbalimbali, kama vile kujikata-kata, kujichoma kwa moto, kujichubua, au kujikwaruza ngozi.

      c Ukishindwa kuzungumza na mtu uso kwa uso, jaribu kumwandikia barua au kumpigia simu. Mara nyingi, kuzungumza na mtu ni hatua ya kwanza ya kuondolea mbali maumivu ya moyoni.

      d Unaweza kupata habari zaidi kuhusu kushuka moyo, katika Buku la 1, sura ya 13.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki