Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Vita Vilivyobadili Maisha Yangu
    Amkeni!—2005 | Oktoba 22
    • Mabadiliko ya Mgawo

      Nilipewa mgawo wa kwenda Guatemala, Amerika ya Kati, ambako nilitumikia nikiwa mmishonari kwa mwaka mmoja hivi. Kisha nikaalikwa kufanya kazi ya kuchapisha katika matbaa ndogo kwenye ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova katika mji mkuu, Guatemala City. Mnamo 1981, nilimwoa Lupita, painia mwenyeji, naye akaalikwa kujiunga nami kwenye ofisi ya tawi. Baadaye mnamo 1996, tuliacha kuchapisha vichapo nchini Guatemala tulipoanza kupokea vichapo vyetu vyote kutoka kwenye ofisi ya tawi ya Mexico.

      Binti yetu mdogo, Stephanie, alizaliwa mwaka wa 1984, hata hivyo niliendelea kutumikia kwenye ofisi ya tawi. Niliendelea kutumikia huko pia hata baada ya Lupita kujifungua Mitchell mwaka wa 1987. Haijawa rahisi kuishi mbali na ofisi ya tawi na kusafiri kila siku umbali wa kilometa kumi hivi. Lakini limekuwa pendeleo kutumikia kwenye ofisi ya tawi, na familia yangu imeniunga mkono kwa dhati.

      Sasa Lupita na Stephanie ni mapainia, naye Mitchell ni mhudumu aliyebatizwa. Atamaliza masomo yake kwenye chuo cha ufundi mwaka huu, na ana mradi wa kufuatia huduma ya wakati wote. Ninajua kwamba tuna mapendeleo haya ya pekee, si kwa sababu ya vipawa vyetu, bali kwa sababu ya fadhili zisizostahiliwa za Yehova. Yeye ni Mungu mwenye upendo, na atamtumia yeyote aliye na nia na anayetegemea mwongozo wake.

      Nyakati nyingine sisi huulizwa tunawezaje kuwa katika huduma ya wakati wote na wakati huohuo kujitegemeza. Sisi hufanya kazi tunapokuwa likizoni. Lakini mbali na hayo, sikuzote tumejaribu kuwa na ‘jicho rahisi’ kuhusiana na vitu vya kimwili, huku tukimtegemea Yehova atusaidie, tukimtumaini, na kutafuta mwongozo wake daima.—Mathayo 6:25-34; Methali 3:5.

      Kubeba bunduki kulifanya nihisi kuwa na mamlaka, kwa hiyo mimi hujaribu kusitawisha unyenyekevu daima. Mfumo wa mambo wa Shetani ulinifunza kuchukia, kuua, kushuku watu, kuwa mwenye jeuri, na mwenye kujitetea. Lakini Yehova amenionyesha rehema na fadhili zenye upendo na ninamshukuru sana kwa jambo hilo. Sasa nimeazimia kuendelea kutojifunza vita tena na kuwapenda na kuwahurumia watu wote.—Mathayo 5:43-45; Isaya 2:4.

      Haijawa rahisi kufanya mabadiliko. Hata hivyo, nimejifunza kuishi maisha yenye amani zaidi. Kwa msaada wa Mungu nimefaulu pia kukabiliana na ndoto mbaya zinazosababishwa na mambo niliyojionea vitani. Ninatazamia kwa hamu wakati ambapo vita havitakuwepo. (Zaburi 46:9) Hadi wakati huo ufike, ninashukuru kwa kupata pendeleo la kutumikia katika kazi inayookoa uhai ya kusaidia watu wajifunze kumhusu Mpaji wetu mkuu wa uhai, Yehova Mungu.

  • Vita Vilivyobadili Maisha Yangu
    Amkeni!—2005 | Oktoba 22
    • [Picha katika ukurasa wa 15]

      Nikiendesha mashini ya kuchapisha katika ofisi ya tawi ya Guatemala, 1982

      [Picha katika ukurasa wa 15]

      Leo, nikiwa na Lupita, Mitchell, na Stephanie

      [Picha katika ukurasa wa 15]

      Nikihubiri na mke wangu

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki