-
Gutenberg—Jinsi Alivyounufaisha Ulimwengu!Amkeni!—1998 | Novemba 8
-
-
Katika mawazo yake Gutenberg aliona kwamba vitu fulani vilitokezwa kwa idadi kubwa, kila kimoja kikifanana na kingine. Mathalani, sarafu zilipigwa chapa, na risasi zilimiminwa katika kalibu ya metali. Kwa hiyo kwa nini kurasa nyingi zinazofanana zisichapishwe na kisha kupanga kurasa kwa utaratibu wa nambari na kuwa vitabu vinavyofanana? Vitabu gani? Alifikiri juu ya Biblia, kitabu ghali sana ambacho ni wachache waliopendelewa ndio waliokuwa na nakala za kibinafsi. Gutenberg alikusudia kutokeza Biblia nyingi zinazofanana, kukizifanya ziwe za bei nafuu zaidi kuliko nakala zilizoandikwa kwa mkono bila kuondoa umaridadi wake wowote. Jambo hili lingefanywaje?
-
-
Gutenberg—Jinsi Alivyounufaisha Ulimwengu!Amkeni!—1998 | Novemba 8
-
-
Uchapishaji Bora
Karakana ya Gutenberg iliyoajiri kati ya watu 15 hadi 20, ilimaliza kuchapisha Biblia ya kwanza katika mwaka wa 1455. Nakala zipatazo 180 zilifanyizwa. Kila Biblia ilikuwa na kurasa 1,282, na mistari 42 kwa kila ukurasa, uliochapishwa katika safu mbili. Kujalidiwa kwa vitabu hivyo—kila Biblia ilikuwa na mabuku mawili—na madoido ya vichwa vilivyopakwa rangi kwa mkono na herufi ya kwanza ya kila sura kulifanywa baadaye katika karakana nyinginezo.
Je, twaweza kuwazia ni vipande vingapi vya chapa vilivyohitajiwa ili kuchapisha Biblia? Kila ukurasa una herufi zipatazo 2,600. Tukichukua kwamba Gutenberg alikuwa na watayarishaji-chapa sita, kila mmoja akifanyia kazi kurasa tatu mara moja, wangehitaji vipande vipatavyo 46,000 vya chapa. Twaweza kuelewa kwa utayari kwamba kalibu ya Gutenberg ilichangia sana kuchapisha kwa kutumia herufi zinazosonga.
Watu walishangaa walipolinganisha Biblia hizo: Kila neno lilikuwa mahali palepale. Jambo hilo halingewezekana kwa hati zilizoandikwa kwa mkono. Günther S. Wegener aandika kwamba Biblia hiyo yenye mistari 42 ilikuwa na “usare na ulinganifu, upatano na umaridadi, hivi kwamba wachapishaji katika miaka yote walishangazwa na ubora wa kazi hiyo.”
Maangamizi ya Kifedha
Hata hivyo, Fust alipendezwa zaidi na pesa kuliko kazi bora. Ilichukua muda mrefu kuliko alivyotarajia kupata faida kutokana na kitega-uchumi chake. Wenzi hao wakaachana, na katika mwaka wa 1455—wakati tu Biblia zilipokuwa zikikamilishwa—Fust akakataa kutoa mikopo. Gutenberg hakuweza kulipa mkopo na akapoteza kesi ya mahakamani iliyofuata. Alilazimishwa kusalimisha kwa Fust angalau vifaa fulani vya kuchapishia na chapa kwa ajili ya Biblia. Fust alifungua kiwanda chake cha kuchapisha pamoja na mfanyakazi stadi wa Gutenberg Peter Schöffer. Biashara yao, Fust na Schöffer, ilitambuliwa kwa kazi bora ambayo kwa kweli ilikuwa ya Gutenberg na ikawa matbaa ya biashara ya kwanza yenye mafanikio ulimwenguni.
-
-
Gutenberg—Jinsi Alivyounufaisha Ulimwengu!Amkeni!—1998 | Novemba 8
-
-
Nakala Zilizookoka za Biblia ya Gutenberg
Ni Biblia ngapi za Gutenberg zilizookoka? Mpaka hivi majuzi iliaminiwa kuwa zilikuwa 48—nyinginezo zikiwa hazijakamilishwa—zikiwa zimesambaa kote katika Ulaya na Amerika ya Kaskazini. Mojawapo ya nakala nzuri zaidi ni Biblia ya hati ya ngozi katika Maktaba ya Congress katika Washington, D.C. Kisha, katika mwaka wa 1996, uvumbuzi wenye kugusa hisia ulifanywa: Kisehemu zaidi cha Biblia ya Gutenberg kiligunduliwa katika hifadhi ya vitu vya kale ya kanisa katika Rendsburg, Ujerumani.—Ona Amkeni! la Januari 22, 1998, ukurasa wa 29.
Jinsi tunavyoweza kuwa wenye shukrani kwamba sasa Biblia inaweza kupatikana kwa mtu yeyote! Bila shaka, hii haimaanishi kwamba tunaweza kwenda na kununua Biblia ya mistari 42 ya Gutenberg! Moja ina thamani ya kiasi gani? Jumba la Makumbusho la Gutenberg katika Mainz lilijipatia nakala moja katika mwaka wa 1978 kwa deutsche mark milioni 3.7 (leo ni dola zipatazo milioni 2). Biblia hiyo sasa ina thamani inayopita kiasi hicho mara kadhaa.
Ni nini kinachoifanya Biblia ya Gutenberg iwe ya kipekee? Profesa Helmut Presser, aliyekuwa mkurugenzi wa hapo awali wa Jumba la Makumbusho la Gutenberg alidokeza sababu tatu. Kwanza, Biblia ya Gutenberg ilikuwa kitabu cha kwanza kuchapishwa katika Magharibi kikiwa na herufi zinazosonga. Pili, ilikuwa Biblia ya kwanza kupata kuchapishwa. Tatu, ina umaridadi wa kustaajabisha. Profesa Presser aandika kwamba katika Biblia ya Gutenberg, twaona “kiwango cha juu kabisa cha maandishi aina ya Gothic.”
-