-
Ufunuo na WeweUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Wenye furaha ni wale ambao hufua majoho yao ili mamlaka ya kwenda kwenye miti ya uhai imkini kuwa yao na kwamba wao wamkini kupata mwingilio ndani ya jiji kupitia malango yalo.
-
-
Ufunuo na WeweUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
8. (a) Ni nani pekee ‘wanaokwenda kwenye miti ya uhai,’ na hili humaanisha nini? (b) Umati mkubwa ‘umefuaje majoho yao,’ na wanadumishaje msimamo safi?
8 Ni wale Wakristo wapakwa-mafuta pekee ambao “hufua majoho yao” kikweli ili wawe safi machoni pa Yehova ndio wanaopendelewa “kwenda kwenye miti ya uhai.” Yaani, wanapokea haki na cheti cha kuwa na uhai usioweza kufa katika cheo chao cha kimbingu. (Linga Mwanzo 3:22-24; Ufunuo 2:7; 3:4, 5.) Baada ya kifo chao wakiwa binadamu, wanapata mwingilio ndani ya Yerusalemu Jipya kwa ufufuo. Malaika 12 wanawaruhusu kuingia ndani, huku wakizuia wowote wanaozoea uwongo au utovu wa usafi ingawa wanadai kuwa na tumaini la kimbingu. Umati mkubwa duniani pia ‘umefua majoho yao na kuyafanya meupe katika damu ya Mwana-Kondoo’ na huhitaji kudumisha msimamo wao safi. Wanaweza kufanya hivyo kwa kuepuka maovu ambayo Yehova anaonya juu yayo hapa, pamoja na kuzingatia moyoni onyo la Yesu katika jumbe zake saba kwa makundi.—Ufunuo 7:14, NW; sura 2 na 3.
-