-
Kasirani ya Mungu Yaletwa Kwenye TamatiUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“Tazama! Mimi ninakuja kama mwivi. Mwenye furaha ni mmoja ambaye hukaa ameamka na kutunza mavazi yake ya nje, ili asipate kutembea uchi na watu watazame aibu yake.” (Ufunuo 16:15, NW)
-
-
Kasirani ya Mungu Yaletwa Kwenye TamatiUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
28. Yesu alitoa onyo gani juu ya kukinza mibano ya ulimwengu, na “siku hiyo” ni ipi ambayo Wakristo hawataki iwe juu yao “kama tanzi”?
28 Yesu alionya pia juu ya aina ya mibano ambayo ulimwengu huu, wenye kulowa propaganda, ungetia juu ya Wakristo. Alisema: “Toeni uangalifu kwa nyinyi wenyewe kwamba mioyo yenu isipate kulemewa kamwe na kula kupita kiasi na kunywa sana na wasiwasi wa maisha, na ghafula siku hiyo iwe juu ya nyinyi papo hapo kama tanzi. . . . Fulizeni kuamka, basi, wakati wote mkifanya dua kwamba nyinyi mpate kufaulu katika kuponyoka vitu hivi vyote ambavyo vimekusudiwa kutukia, na katika kusimama mbele ya Mwana wa binadamu.” (Luka 21:34-36, NW) “Siku hiyo” ni “ile siku kubwa ya Mungu Mweza Yote.” (Ufunuo 16:14, NW) Kadiri “siku hiyo” ya kutetewa kwa enzi kuu ya Yehova ikaribiavyo, inazidi kuwa vigumu zaidi kupambana kwa kufaulu na “wasiwasi wa maisha.” Wakristo wanahitaji kuwa chonjo na wenye kutazama, wakikaa hali wameamka mpaka siku hiyo iwasilipo.
29, 30. (a) Ni nini kinachodokezwa na onyo la Yesu kwamba wale wanaopatikana wakilala wangeona aibu kwa kupoteza “mavazi ya nje” yao? (b) “Mavazi ya nje” yanamtambulisha mvaaji kuwa nini? (c) Mtu anaweza kupotezaje mavazi yake ya nje ya ufananisho, na tokeo likiwa nini?
29 Ingawa hivyo, ni nini kinachodokezwa na onyo la kwamba wale wanaopatikana wakilala wangeona aibu kwa kupoteza “mavazi ya nje” yao? Katika Israeli wa kale, kuhani au Mlawi yeyote aliyekuwa katika kazi ya lindo kwenye hekalu alikuwa na daraka zito. Waelezaji Wayahudi hutuambia kwamba ikiwa yeyote alikutwa akilala akiwa katika kazi kama hiyo, mavazi yake yangeweza kuvuliwa kutoka kwake na kuchomwa, hivi kwamba aliaibishwa hadharani.
30 Yesu anaonya hapa kwamba jambo kama hilo laweza kutukia leo. Makuhani na Walawi walikuwa kivuli cha ndugu wapakwa-mafuta wa Yesu. (1 Petro 2:9) Lakini kwa upanuzi onyo la Yesu linatumika vilevile kuhusu umati mkubwa. Hapa mavazi ya nje yanayorejezewa hutambulisha mvaaji kuwa Shahidi Mkristo wa Yehova. (Linga Ufunuo 3:18; 7:14.) Ikiwa wowote wanaruhusu mibano ya ulimwengu wa Shetani iwabembeleze walale usingizi au waingie ndani ya kutotenda, wao wanaelekea kupoteza mavazi ya nje, kwa maneno mengine, wapoteze utambulisho wao safi wa kuwa Wakristo. Hali kama hiyo ingekuwa yenye aibu. Ingemweka mmoja katika hatari ya kupoteza kabisa kila kitu.
-