-
Jamhuri Ya Kidemokrasia Ya Kongo (Kinshasa)2004 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
-
-
Ndugu Heuse alianza kufanya kazi mara moja. Ofisi ya tawi ya Brazzaville ilimwazima projekta na sinema. Halafu alionyesha sinema yenye kichwa Furaha ya Jamii ya Ulimwengu Mpya (The Happiness of the New World Society) kwenye makutaniko ya Léopoldville, na aliwaonyesha pia maofisa fulani wa serikali sinema hiyo. Iliwasaidia sana akina ndugu na watu wanaopendezwa kutambua kwamba Mashahidi wana undugu wa kimataifa na wote wanaishi kwa amani na furaha. Walishangaa sana kumwona ndugu Mwafrika akiwabatiza Wazungu. Meya wa Léopoldville aliifurahia sana sinema hiyo hata akasema: “Kazi hii [ya Mashahidi wa Yehova] inapaswa kuendelezwa kadiri iwezekanavyo.” Watu wapatao 1,294 walihudhuria maonyesho manne ya kwanza.
-
-
Jamhuri Ya Kidemokrasia Ya Kongo (Kinshasa)2004 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
-
-
[Picha katika ukurasa wa 186]
Wakongomani wengi walifurahi kuwaona watu wakibatizwa kwenye makusanyiko ya kimataifa yaliyoonyeshwa katika sinema “Furaha ya Jamii ya Ulimwengu Mpya”
-