Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Iweni Wavunaji Wenye Furaha!
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Julai 15
    • Waliotumwa Kuwa Wavunaji

      3. Wafuasi wa mapema wa Yesu walipata furaha katika njia gani?

      3 Maisha ya wavunaji wa mapema—hasa mitume 11 wa Yesu waliokuwa waaminifu—yalibadilika sana mwaka wa 33 W.K., siku walipoenda mlimani huko Galilaya kuonana na Kristo aliyekuwa amefufuliwa. (Mathayo 28:16) Huenda “zaidi ya ndugu mia tano” walikuwepo pindi hiyo. (1 Wakorintho 15:6) Walikuwa wangali wanakumbuka kazi ambayo Yesu aliwaagiza wafanye. Aliwaambia: “Nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, kuwabatiza katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu, kuwafundisha kushika mambo yote ambayo mimi nimewaamuru nyinyi.” (Mathayo 28:19, 20) Licha ya mnyanyaso mkali, walipata furaha nyingi katika kazi ya kuvuna walipoona makutaniko ya wafuasi wa Kristo yakianzishwa mahali kwingi. Baada ya muda, ‘habari njema ikahubiriwa katika viumbe vyote chini ya mbingu.’—Wakolosai 1:23; Matendo 1:8; 16:5.

      4. Wanafunzi wa Kristo walitumwa chini ya hali gani?

      4 Awali katika huduma yake huko Galilaya, Yesu alikuwa amewaita mitume wake 12 na kuwatuma hasa wakatangaze hivi: “Ufalme wa mbingu umekaribia.” (Mathayo 10:1-7) Yeye mwenyewe ‘aliondoka ili kutalii majiji na vijiji vyote vya Galilaya, akifundisha katika masinagogi yao na kuhubiri habari njema ya ufalme na kuponya kila namna ya maradhi na kila namna ya udhaifu.’ Yesu alihurumia umati “kwa sababu ulikuwa umechunwa ngozi na kutupwa huku na huku kama kondoo wasio na mchungaji.” (Mathayo 9:35, 36) Kisha akiwa ameguswa moyo sana akawaambia wanafunzi wake: “Ndiyo, mavuno ni mengi, lakini wafanyakazi ni wachache. Kwa hiyo, ombeni Bwana-mkubwa wa mavuno [Yehova Mungu] atume wafanyakazi katika mavuno yake.” (Mathayo 9:37, 38) Miezi sita tu kabla ya kumaliza huduma yake duniani, Yesu aliona kulikuwa na uhitaji wa kuwa na wavunaji huko Yudea pia. (Luka 10:2) Katika pindi zote mbili, aliwatuma wafuasi wake wafanye kazi ya kuvuna.—Mathayo 10:5; Luka 10:3.

  • Iweni Wavunaji Wenye Furaha!
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Julai 15
    • 6. Mitume walifanya kazi gani katika karne ya kwanza?

      6 Kufikia katikati ya karne ya kwanza, mtume Paulo alikuwa na shughuli nyingi za kuhubiri habari njema. Hapana shaka alifanikiwa katika kazi yake ya kuvuna, kwa kuwa alipowaandikia Wakristo wa Korintho yapata mwaka wa 55 W.K., alisema: “Nawajulisha nyinyi, akina ndugu, habari njema niliyowatangazia, mliyoipokea pia, ambayo katika hiyo mwasimama pia.” (1 Wakorintho 15:1) Mitume na Wakristo wengine wa mapema walikuwa wavunaji wenye bidii. Ingawa Biblia haituambii ni mitume wangapi waliookoka matukio yenye kuogofya yaliyomalizika kwa kuharibiwa kwa Yerusalemu mwaka wa 70 W.K., tunajua kwamba mtume Yohana alikuwa bado anahubiri miaka 25 hivi baadaye.—Ufunuo 1:9.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki