-
“Mtu Mwerevu Huzifikiria Njia Zake”Mnara wa Mlinzi—2005 | Julai 15
-
-
lakini mtu mwenye uwezo wa kufikiri huchukiwa.”—Methali 14:16, 17.
-
-
“Mtu Mwerevu Huzifikiria Njia Zake”Mnara wa Mlinzi—2005 | Julai 15
-
-
Lakini kwa nini mtu mwenye uwezo wa kufikiri huchukiwa?
Usemi wa awali unaotafsiriwa “uwezo wa kufikiri” una maana mbili. Unapotumiwa kwa njia inayofaa, usemi huo unaweza kumaanisha utambuzi au werevu. (Methali 1:4; 2:11; 3:21) Lakini unapotumiwa katika njia isiyofaa, unaweza kumaanisha maoni maovu au mawazo mabaya sana.—Zaburi 37:7; Methali 12:2; 24:8.
Ikiwa usemi “mtu mwenye uwezo wa kufikiri” unamaanisha mtu anayepanga hila mbovu, ni rahisi kuelewa ni kwa nini mtu kama huyo huchukiwa. Hata hivyo, mtu mwenye utambuzi anaweza pia kuchukiwa na wale wasio na sifa hiyo. Kwa mfano, wale wanaotumia uwezo wao wa kufikiri na kuchagua ‘kutokuwa sehemu ya ulimwengu,’ huchukiwa na ulimwengu. (Yohana 15:19) Vijana Wakristo ambao hutumia uwezo wao wa kufikiri na kukataa kushawishiwa na vijana wenzao kufanya mambo yasiyofaa hudhihakiwa. Ukweli ni kwamba waabudu wa kweli huchukiwa na ulimwengu ambao unakaa katika nguvu za Shetani Ibilisi.—1 Yohana 5:19.
-