Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Wakati wa Kupenda na Wakati wa Kuchukia”
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Desemba 1
    • Tutazungumzia maana hiyo ya pili. Chuki hiyo ni kutopendezwa kabisa, bali si wivu wenye chuki, uadui, au tamaa ya kusababisha madhara. Je, Mungu anaweza kuwa na chuki ya aina hiyo? Ona maneno yaliyoandikwa kwenye Methali 6:16-19: “Kuna vitu sita ambavyo Yehova huchukia; naam, vitu saba vinachukiza nafsi yake: macho ya majivuno, ulimi wa uwongo, na mikono inayomwaga damu isiyo na hatia, moyo unaotunga hila zenye kuumiza, miguu iliyo myepesi kukimbilia ubaya, shahidi wa uwongo anayesema uwongo, na yeyote anayetokeza magomvi kati ya ndugu.”

      Kama tunavyoona, kuna matendo fulani ambayo Mungu anachukia. Lakini si lazima amchukie mtu anayetenda mambo hayo. Anaona hali zinazomsukuma mtu atende kwa njia hiyo, kama vile, udhaifu wa kimwili, mazingira, malezi, na kutojua. (Mwanzo 8:21; Waroma 5:12)

  • “Wakati wa Kupenda na Wakati wa Kuchukia”
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Desemba 1
    • Chuki Inayofaa

      Namna gani ikiwa mtu anajua mapenzi ya Mungu lakini akatae kuyafanya? Mtu huyo hataonyeshwa upendo na Mungu, bali atakosa kibali chake. Akizoea kutenda kimakusudi mambo ambayo Yehova anachukia, Mungu atamchukia. Kwa mfano, Biblia inasema: “Yehova humchunguza mwadilifu na pia mwovu, na mtu yeyote anayependa jeuri nafsi Yake hakika inamchukia.” (Zaburi 11:5) Mtu kama huyo asiyetubu hawezi kusamehewa, kama vile mtume Paulo anavyosema waziwazi katika barua yake kwa Waebrania: “Tukizoea kutenda dhambi kimakusudi baada ya kupokea ujuzi sahihi juu ya kweli, hakuna tena dhabihu yoyote iliyobaki kwa ajili ya dhambi, lakini kuna tarajio hakika lenye kuogopesha la hukumu na kuna wivu unaowaka moto ambao utawateketeza wale wanaopinga.” (Waebrania 10:26, 27) Kwa nini Mungu mwenye upendo anachukua msimamo huo?

      Mtu akizoea kutenda dhambi nzito kimakusudi, uovu unaweza kutia mizizi kabisa ndani yake hivi kwamba mtu huyo hawezi kuuacha. Anaweza kuwa mpotovu, mzoefu, asiyeweza kubadilika. Biblia inamlinganisha mtu huyo na chui ambaye hawezi kubadili madoa yake. (Yeremia 13:23) Kwa vile hawezi kutubu, mtu huyo anafanya ile ambayo Biblia inaiita “dhambi ya milele,” ambayo haina msamaha.—Marko 3:29.

      Ndivyo ilivyokuwa kwa Adamu na Hawa na pia kwa Yuda Iskariote. Kwa kuwa Adamu na Hawa waliumbwa wakiwa wakamilifu na kwa vile amri ambayo Mungu aliwapa ilikuwa wazi na wote wawili waliielewa, bila shaka walitenda dhambi kwa kupenda na kimakusudi na hivyo hawangesamehewa. Baadaye Mungu alipozungumza nao hakuwapa nafasi ya kutubu. (Mwanzo 3:16-24) Ingawa Yuda hakuwa mkamilifu, alikuwa ameshirikiana kwa ukaribu na Mwana wa Mungu na bado akawa msaliti. Yesu mwenyewe alimwita “mwana wa maangamizi.” (Yohana 17:12) Pia, Biblia inaonyesha kwamba Ibilisi amekuwa akitenda dhambi kimakusudi kwa muda mrefu na anangojea tu kuangamizwa. (1 Yohana 3:8; Ufunuo 12:12) Wote hao walifanya Mungu awachukie.

      Hata hivyo, inapendeza kujua kwamba miongoni mwa watu ambao wametenda dhambi kuna wale ambao wanaweza kusamehewa. Yehova ni mwenye subira sana na hafurahii kuwaadhibu wale ambao wametenda dhambi kwa sababu ya kutojua. (Ezekieli 33:11) Anawapa nafasi ya kutubu ili wasamehewe. Tunasoma hivi: “Mtu mwovu aiache njia yake, na mtu mwenye madhara ayaache mawazo yake; naye arudi kwa Yehova, ambaye atamwonyesha rehema, na kwa Mungu wetu, kwa maana atasamehe kwa njia kubwa.”—Isaya 55:7.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki