-
Kufunika Kichwa—Wakati Gani na kwa Nini?“Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
-
-
Kwa mfano, akilazimika kuongoza funzo la Biblia mume wake akiwapo, atatambua mamlaka ya mume wake kwa kufunika kichwa chake. Atafanya hivyo, iwe mume wake amebatizwa au hajabatizwa, kwa kuwa mume ndiye kichwa cha familia.a Ikiwa anahitaji kufundisha au kusali mtoto wake wa kiume aliyebatizwa akiwapo, atafunika kichwa pia, si kwa sababu mwana huyo ni kichwa cha familia, bali kwa sababu ya mamlaka ambayo wanaume waliobatizwa wamepewa katika kutaniko la Kikristo.
-
-
Kufunika Kichwa—Wakati Gani na kwa Nini?“Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
-
-
Au anaweza kuongoza funzo la Biblia lililopangwa mapema, akiwa ameandamana na mwanamume aliyebatizwa. Kwa kuwa shughuli hizo ni sehemu ya utendaji wa kutaniko la Kikristo, anapaswa kufunika kichwa ili kuonyesha kwamba anashughulikia jukumu ambalo kwa kawaida hushughulikiwa na mwanamume.
-