-
“Kiongozi Wenu Ni Mmoja, Kristo”Mnara wa Mlinzi—2010 | Septemba 15
-
-
Mwangalizi wa Kutaniko la Kikristo
7. Yesu analiongoza kutaniko la Kikristo kupitia nini?
7 Muda mfupi kabla ya kupanda mbinguni, Yesu aliyefufuliwa aliwaambia hivi wanafunzi wake: “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.” (Mt. 28:18) Kwa uwezo wa Yehova, Yesu aliwapa wanafunzi wake roho takatifu ili iwatie nguvu katika kweli ya Kikristo. (Yoh. 15:26) Yesu aliwamiminia roho hiyo Wakristo wa mapema siku ya Pentekoste ya mwaka wa 33 W.K. (Mdo. 2:33) Kutaniko la Kikristo lilianzishwa wakati huo ambao roho takatifu ilimiminwa. Huko mbinguni, Yehova alimweka Mwana wake kuwa kiongozi juu ya kutaniko lote duniani. (Soma Waefeso 1:22; Kol. 1:13, 18.) Yesu analiongoza kutaniko la Kikristo kupitia roho takatifu ya Yehova, na ana malaika ambao ‘walitiishwa kwake.’—1 Pet. 3:22.
8. Katika karne ya kwanza, Kristo alitumia nani duniani ili kuwaongoza wanafunzi wake, na anatumia nani leo?
8 Pia, kupitia roho takatifu, Kristo alitoa “zawadi katika wanadamu,” wengine ‘wakiwa wachungaji na walimu’ katika kutaniko. (Efe. 4:8, 11) Mtume Paulo aliwahimiza hivi waangalizi Wakristo: “Jiangalieni ninyi wenyewe na kundi lote, ambalo roho takatifu imewaweka ninyi rasmi kuwa waangalizi kati yake, kulichunga kutaniko la Mungu.” (Mdo. 20:28) Kutaniko la Kikristo lilipoanza, waangalizi hao wote walikuwa wanaume waliotiwa mafuta kwa roho. Mitume na wazee wa kutaniko la Yerusalemu walikuwa baraza linaloongoza. Kristo aliwatumia kuongoza kundi lote la “ndugu” zake watiwa-mafuta duniani. (Ebr. 2:11; Mdo. 16:4, 5) Katika wakati huu wa mwisho, Kristo amemkabidhi “mali zake zote,” yaani, faida zake zote za Ufalme duniani, “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” na mwakilishi wa mtumwa huyo, Baraza Linaloongoza, ambacho ni kikundi cha wanaume Wakristo watiwa-mafuta. (Mt. 24:45-47) Watiwa-mafuta na waandamani wenzao, kondoo wengine, wanatambua kwamba wanapofuata uongozi wa Baraza Linaloongoza la siku zetu, kwa kweli wanamfuata Kiongozi wao, Kristo.
-
-
“Kiongozi Wenu Ni Mmoja, Kristo”Mnara wa Mlinzi—2010 | Septemba 15
-
-
Uongozi wa Yesu Juu ya Kutaniko Lake
12, 13. Kitabu cha Ufunuo kinaonyesha jinsi gani kwamba Kristo anachunguza kwa makini mambo yanayotendeka katika kila kutaniko?
12 Yesu alichunguza kwa makini mambo yaliyokuwa yakitendeka katika makutaniko ya wafuasi wake watiwa-mafuta katika karne ya kwanza W.K. Alijua vizuri sana hali ya kiroho ya kila kutaniko. Jambo hilo linaonekana wazi hasa tunaposoma Ufunuo sura ya 2 na ya 3. Anataja makutaniko saba yaliyo katika Asia Ndogo. (Ufu. 1:11) Tuna kila sababu ya kuamini kwamba alijua pia hali ya kiroho ya makutaniko mengine ya wafuasi wake yaliyokuwa duniani wakati huo.—Soma Ufunuo 2:23.
13 Yesu aliyapongeza makutaniko mengine kwa sababu ya uvumilivu wao, uaminifu chini ya majaribu, ushikamanifu kwa neno lake, na kwa kuwakataa waasi-imani. (Ufu. 2:2, 9, 13, 19; 3:8) Kwa upande mwingine, alitoa mashauri makali kwa makutaniko fulani kwa sababu upendo wao kumwelekea ulikuwa umepoa, pia yaliruhusu ibada ya sanamu, uasherati, na madhehebu kati yao. (Ufu. 2:4, 14, 15, 20; 3:15, 16) Akiwa mwangalizi wa kiroho mwenye upendo, hata kwa wale ambao aliwashauri kwa ukali, Yesu alisema hivi: “Wale wote ninaowapenda, mimi huwakaripia na kuwatia nidhamu. Kwa hiyo uwe mwenye bidii na utubu.” (Ufu. 3:19) Ingawa alikuwa mbinguni, Yesu alikuwa akiyaongoza makutaniko ya wanafunzi wake duniani kupitia roho takatifu. Mwishoni mwa ujumbe mbalimbali kwa makutaniko hayo, alisema hivi: “Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo roho inayaambia makutaniko.”—Ufu. 3:22.
-