-
Mtumikie Mungu wa UhuruMnara wa Mlinzi—2012 | Julai 15
-
-
SALI ILI UWE NA MOYO WENYE HEKIMA NA MTIIFU
10. Kwa nini tunapaswa kujitahidi kumwiga Mfalme Sulemani alipokuwa kijana?
10 Alipokuwa angali kijana, Sulemani alisali hivi kwa unyenyekevu: ‘Mimi ni mvulana mdogo tu. Sijui jinsi ya kutoka na jinsi ya kuingia.’ Kisha akasali ili apewe moyo wenye hekima na mtiifu. (1 Fal. 3:7-9, 12) Yehova alijibu ombi hilo la unyoofu, na atajibu ombi lako pia, iwe wewe ni kijana au mzee. Bila shaka, Yehova hatakupa ufahamu na hekima kimuujiza. Lakini atakufanya uwe mwenye hekima ukijifunza kwa bidii Neno lake, ukisali ili akupe roho takatifu, na kunufaika kikamili na maandalizi ya kiroho ambayo anatoa kupitia kutaniko la Kikristo. (Yak. 1:5) Kwa kweli, Yehova anatumia njia hizo kuwafanya hata watumishi wake vijana wawe na hekima zaidi kuliko wale wote wanaopuuza mashauri yake, hata wale wanaoitwa eti “wenye hekima na walio na akili” katika ulimwengu huu.—Luka 10:21; soma Zaburi 119:98-100.
-
-
Mtumikie Mungu wa UhuruMnara wa Mlinzi—2012 | Julai 15
-
-
15. Utajuaje ikiwa unasitawisha moyo wenye hekima na mtiifu?
15 Utajuaje ikiwa unasitawisha moyo wenye hekima na mtiifu? Njia moja ni kulinganisha njia yako ya kufikiri na ile ya watu waaminifu walioishi zamani, kama vile Mfalme Daudi, aliyeandika hivi: “Ee Mungu wangu, nimependezwa na kufanya mapenzi yako, na sheria yako imo ndani yangu.” (Zab. 40:8) Pia, mwandikaji wa Zaburi 119 alisema hivi: “Jinsi ninavyoipenda sheria yako! Ndiyo ninayoihangaikia mchana kutwa.” (Zab. 119:97) Upendo wa aina hiyo haukui kwenye udongo usio na kina. Badala yake, unatokana na kujifunza kwa undani, kusali, kutafakari, na uzoefu, yaani, kuhesabu baraka nyingi sana ambazo umepata maishani kwa sababu ya kushikamana na viwango vya Mungu.—Zab. 34:8.
-