-
Jinsi Wema Utakavyoshinda UovuMnara wa Mlinzi—2006 | Januari 1
-
-
Mwelekeo wa Kutenda Mabaya
Mfalme Daudi mwenyewe alionyesha mojawapo ya sababu za matendo maovu. Baada ya matendo yake mabaya kujulikana, alikubali makosa yake. Aliandika hivi baada ya kutubu: “Tazama! Nilizaliwa kwa maumivu nikiwa na kosa, na mama yangu alinichukua mimba katika dhambi.” (Zaburi 51:5) Mungu hakukusudia kamwe akina mama wazae watoto ambao wangekuwa watenda-dhambi. Hata hivyo, Hawa na Adamu walipochagua kumwasi Mungu, walipoteza uwezo wao wa kuzaa watoto wasio na dhambi. (Waroma 5:12) Jamii ya wanadamu wasio wakamilifu ilipoendelea kuongezeka, sasa ilionekana wazi kwamba “mwelekeo wa moyo wa mwanadamu ni mbaya tangu ujana wake na kuendelea.”—Mwanzo 8:21.
Mwelekeo huo wa kutenda mabaya usipodhibitiwa, unaweza kuongoza kwenye “uasherati, . . . uadui, mizozo, wivu, milipuko ya hasira, magomvi, migawanyiko, madhehebu, husuda,” na tabia nyingine zenye kuharibu ambazo Biblia inazitaja kuwa “matendo ya mwili.” (Wagalatia 5:19-21) Kuhusu kisa cha Mfalme Daudi, ni wazi kwamba alishindwa na udhaifu wa mwili naye akafanya uasherati, ambao ulisababisha mizozo. (2 Samweli 12:1-12) Angeweza kushinda mwelekeo wake wa ukosefu wa adili. Badala yake, kwa kuendelea kumtamani Bath-sheba, Daudi alifuata mwelekeo ambao baadaye ulitajwa hivi na mwanafunzi Yakobo: “Kila mtu hujaribiwa kwa kuvutwa na kushawishiwa na tamaa yake mwenyewe. Kisha tamaa, wakati imetunga mimba, huzaa dhambi; nayo dhambi, wakati imetimizwa, huleta kifo.”—Yakobo 1:14, 15.
Kuuawa kwa watu wengi, kulala wanawake kinguvu, na uporaji wa mali uliotajwa katika makala iliyotangulia ni mifano ya mambo ambayo hutokea watu wanaporuhusu tamaa mbaya ziongoze matendo yao.
-
-
Jinsi Wema Utakavyoshinda UovuMnara wa Mlinzi—2006 | Januari 1
-
-
Kuondolewa kwa Mwelekeo wa Kutenda Mabaya
Ikiwa uovu utakomeshwa katika jamii ya wanadamu, mwelekeo uliorithiwa wa mwanadamu wa kutenda mabaya, ukosefu wa ujuzi sahihi, na uvutano wa Shetani unapaswa kuondolewa. Lakini mwelekeo wa mwanadamu wa kutenda dhambi unaweza kuondolewaje moyoni?
Hakuna jambo lolote ambalo mwanadamu anaweza kufanya ili kuondoa mwelekeo wa kutenda dhambi. Hata hivyo, Yehova Mungu amefanya maandalizi ya kuondoa dhambi iliyorithiwa na kutokamilika kwa wote walio tayari kuyakubali. Mtume Yohana aliandika hivi: “Damu ya Yesu . . . hutusafisha kutoka katika dhambi yote.” (1 Yohana 1:7) Wakati Yesu, mtu mkamilifu, alipotoa uhai wake kwa hiari, “alichukua dhambi zetu katika mwili wake mwenyewe juu ya mti, ili tuachane kabisa na dhambi na kuishi kwa uadilifu.” (1 Petro 2:24) Kifo cha dhabihu cha Yesu kingeondoa madhara ya uovu wa Adamu. Paulo anasema kwamba Kristo Yesu alikuwa “fidia inayolingana kwa ajili ya wote.” (1 Timotheo 2:6) Naam, kifo cha Kristo kilifungua njia ili wanadamu wote wapate tena ukamilifu ambao Adamu alipoteza.
-