-
Iceland2005 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Jengo hilo liliwekwa wakfu Mei 1975, ndugu Milton G. Henschel alipotembelea Iceland na kutoa hotuba ya kuweka wakfu.
-
-
Iceland2005 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Ndugu Henschel alitembelea Iceland kwa mara ya kwanza Mei 1970. Wamishonari kadhaa waliokuwa wamelemewa na usingizi walimkaribisha. Wamishonari hao walikuwa wamelemewa na usingizi si kwa sababu Ndugu Henschel alikuwa amefika asubuhi na mapema, bali kwa sababu walikuwa wamekesha wakitazama volkeno maarufu inayoitwa Hekla, ambayo ilikuwa imeanza kulipuka siku iliyotangulia.
Ndugu Henschel aliwatia moyo wamishonari na mapainia wa pekee hasa. Aliwaalika wote kwenye mkutano wa pekee na kusimulia mambo aliyojionea alipokuwa painia katika ile miaka ambayo uchumi ulikuwa umeshuka sana nchini Marekani. Aliwaeleza jinsi mapainia walivyobadilisha vitabu kwa kuku, mayai, siagi, mboga, miwani, na hata mtoto wa mbwa! Kwa njia hiyo, kazi ilisonga mbele katika nyakati hizo ngumu, nao mapainia hawakukosa mahitaji ya lazima.
Wageni wanaotembelea Iceland wanagundua haraka kwamba chakula ni tofauti na kile ambacho wamezoea. Aina moja ya chakula cha kipekee cha Iceland ni svid, yaani, kichwa cha kondoo kilichokatwa katika sehemu mbili na kuchemshwa. Wazia unatazama sahani yako na kuona nusu ya kichwa cha kondoo kikiwa na meno na jicho moja! Wageni wengi hawapendi hata kukiona. Samaki waliotoka tu kuvuliwa wanapatikana sikuzote. Chakula kingine cha kipekee ni hardfiskur: samaki ambaye ametolewa mifupa na kukaushwa. Samaki huyo hapikwi, bali huliwa pamoja na siagi. Kwa kawaida samaki huyo ni mgumu, na hupondwa ili awe laini. Basi, wamishonari walikuwa na hamu ya kusikia maoni ya Ndugu Henschel kuhusu chakula hicho. Baada ya kukionja wamishonari walimwuliza kama alikipenda. Alifikiri kidogo, kisha akajibu hivi kwa busara: “Sijawahi kula mbao tamu kama hii.”
-