Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Herode Mkuu—Mjenzi Stadi
    Amkeni!—2009 | Septemba
    • Kaisaria—Jiji la Bandarini

      Herode alijenga mojawapo ya bandari kubwa zaidi katika ulimwengu wa Roma huko Kaisaria. Ukubwa wake umewashangaza hata wachimbuaji wa vitu vya kale. Kulikuwa na nafasi ya meli 100 kutia nanga, na hilo linaonyesha kwamba wakati mmoja Kaisaria lilikuwa kituo cha kibiashara cha kimataifa.

      Gati na kuta za kuzuia mawimbi zilijengwa kwa kutumia tekinolojia ya hali ya juu sana. Hata hivyo, wasomi walishangazwa na jinsi ambavyo wafanyakazi wangeweza kubeba mawe makubwa ambayo mwanahistoria Myahudi Flavio Yosefo alisema yalikuwa na urefu wa mita 15 hivi, upana wa mita 3 hivi, na kimo cha mita 3 hivi. Hivi karibuni, wapiga-mbizi wamegundua kwamba mawe ambayo Herode alitumia yametengenezwa kwa zege. Ili wajenge gati na kuta za kuzuia mawimbi, wafanyakazi walimwaga zege katika viunzi vya mbao, na kisha wakaingiza mawe hayo chini ya maji na kuyashindilia.

      Jiji hilo la bandarini lililojengwa kwa mpangilio mzuri sana lilikuwa na hekalu lililowekwa wakfu kwa Kaisari Agusto, jumba la kifalme, kiwanja cha mashindano ya magari yaliyokokotwa na farasi, jumba la maonyesho linaloweza kutoshea watu 4,000, na mfumo wa kuondoa maji-taka wa chini ya ardhi. Mifereji na njia za chini ya ardhi ziliingiza maji baridi jijini Kaisaria kutoka kwenye chemchemi za Mlima Karmeli ulioko umbali wa kilomita 6 hivi.

  • Herode Mkuu—Mjenzi Stadi
    Amkeni!—2009 | Septemba
    • [Picha katika ukurasa wa 25]

      KAISARIA

      Mchoro wa msanii

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki