-
Uwe na Bidii kwa Ajili ya Nyumba ya Yehova!Mnara wa Mlinzi—2009 | Juni 15
-
-
Tutunze Vizuri Mahali Petu pa Mikutano
13. Ni kazi gani ambayo Hezekia alianzisha mwanzoni mwa utawala wake?
13 Katika mwezi wa kwanza wa utawala wake, Hezekia alionyesha kwamba alikuwa na bidii kwa ajili ya ibada ya Yehova kwa kufungua tena hekalu na kulirekebisha. Aliweka makuhani na Walawi ili waisafishe nyumba ya Mungu. Walifanya kazi hiyo kwa muda wa siku 16. (Soma 2 Mambo ya Nyakati 29:16-18.) Jitihada hizo zinatukumbusha kazi tunayofanya ya kutunza na kurekebisha mahali petu pa mikutano ili pawe safi, na hilo linaonyesha kwamba tuna bidii kwa ajili ya ibada ya Yehova. Je, hujawahi kusikia mambo yaliyoonwa yanayoonyesha kwamba watu wanavutiwa na bidii ya ndugu na dada zetu ambao wanashiriki katika kazi hiyo? Ndiyo, jitihada zao zinamletea Yehova sifa nyingi.
-
-
Uwe na Bidii kwa Ajili ya Nyumba ya Yehova!Mnara wa Mlinzi—2009 | Juni 15
-
-
Tii Maagizo ya Mungu
16, 17. Watu wa Mungu wameshiriki kwa bidii katika utendaji gani wa pekee, na kumekuwa na matokeo gani?
16 Zaidi ya kurekebisha hekalu, Hezekia alirudisha maadhimisho ya kila mwaka ya Pasaka ambayo Yehova alikuwa ameamuru. (Soma 2 Mambo ya Nyakati 30:1, 4, 5.) Hezekia na wakaaji wa Yerusalemu walialika taifa lote, na hata wakaaji wa ufalme wa kaskazini kuhudhuria maadhimisho hayo. Wakimbiaji walipeleka barua za mwaliko kotekote nchini.—2 Nya. 30:6-9.
17 Katika miaka ya hivi karibuni, tumeshiriki katika jitihada zinazofanana kidogo na hizo. Tumetumia mialiko iliyochapishwa yenye kuvutia ili kuwaalika watu wa maeneo yetu kukusanyika nasi ili kuadhimisha Mlo wa Jioni wa Bwana, na hivyo kutii amri ya Yesu. (Luka 22:19, 20) Baada ya kupokea maagizo kwenye Mikutano yetu ya Utumishi, tumeshiriki kwa bidii katika kazi hiyo. Na Yehova ametubariki sana. Mwaka jana, Mashahidi wa Yehova milioni saba hivi waligawa mialiko hiyo, na jumla ya watu 17,790,631 walihudhuria!
18. Kwa nini ni jambo la maana sana kwetu kuwa na bidii kwa ajili ya ibada ya kweli?
18 Ilisemwa hivi kumhusu Hezekia: “Alimtegemea Yehova Mungu wa Israeli; na baada yake hapakuwa na yeyote kama yeye kati ya wafalme wote wa Yuda, hata wale waliomtangulia. Naye akaendelea kushikamana na Yehova. Hakugeuka kando na kuacha kumfuata, bali aliendelea kuzishika amri zake ambazo Yehova alimwamuru Musa.” (2 Fal. 18:5, 6) Na tufuate mfano wake. Bidii yetu kwa ajili ya nyumba ya Mungu itatusaidia ‘kuendelea kushikamana na Yehova’ huku tukitazamia uzima wa milele.—Kum. 30:16.
-