Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Unapenda Neno la Mungu Kadiri Gani?
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Novemba 1
    • Mtunga-Zaburi Aliyependa Sheria ya Mungu

      5, 6. Ijapokuwa huenda tusijue jina la mwandikaji wa Zaburi ya 119, twaweza kujifunza nini juu yake kwa kusoma na kutafakari mambo aliyoyaandika?

      5 Kwa hakika mwandikaji wa Zaburi ya 119 alithamini sana Neno la Mungu. Ni nani aliyeandika zaburi hiyo? Mwandikaji huyo hatajwi katika Biblia. Lakini, tunajifunza mambo fulani juu yake kutokana na muktadha, na twajua kwamba alikuwa na matatizo maishani. Baadhi ya watu aliowajua ambao walipaswa kuwa waabudu wa Yehova hawakupenda kanuni za Biblia kama yeye. Lakini, huyo mtunga-zaburi hakuruhusu mtazamo wao umzuie asifanye yaliyo sawa. (Zaburi 119:23) Ikiwa unaishi au kufanya kazi na mtu ambaye haheshimu kanuni za Biblia, unaweza kuona jinsi hali yako inavyofanana na hali ya mtunga-zaburi.

      6 Japo mtunga-zaburi alikuwa mcha Mungu, hakujiona kamwe kuwa mwadilifu. Alikiri wazi kutokamilika kwake. (Zaburi 119:5, 6, 67) Lakini, hakuruhusu dhambi imtawale. “Jinsi gani kijana aisafishe njia yake?” akauliza. Akajibu: “Kwa kutii, akilifuata neno lako.” (Zaburi 119:9) Kisha, akikazia jinsi Neno la Mungu lilivyo na nguvu za kutokeza mema, mtunga-zaburi aliongezea: “Moyoni mwangu nimeliweka neno lako, nisije nikakutenda dhambi.” (Zaburi 119:11) Nguvu iwezayo kutusaidia kuepuka kutenda dhambi dhidi ya Mungu ina uwezo kwelikweli!

  • Unapenda Neno la Mungu Kadiri Gani?
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Novemba 1
    • Mwana-Mfalme Aliyekuwa na Ujasiri wa Kuwa Tofauti

      9. Mfalme Hezekia alikuza mtazamo gani kuhusu Neno la Mungu?

      9 Yaliyomo katika Zaburi ya 119 yanapatana vizuri na mambo tunayojua kuhusu Hezekia alipokuwa angali mwana-mfalme kijana. Wasomi wengine wa Biblia hudokeza kwamba Hezekia ndiye aliyeandika zaburi hii. Ingawa jambo hilo si hakika, twajua kwamba Hezekia aliheshimu sana Neno la Mungu. Kupitia mwenendo wake maishani, alionyesha kwamba alikubaliana kabisa na maneno ya Zaburi 119:97. Biblia yasema hivi juu ya Hezekia: “Alishikamana na BWANA, hakuacha kumfuata, bali alizishika amri zake BWANA alizomwamuru Musa.”—2 Wafalme 18:6.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki