Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Watu Wanasema Kwamba Mimi Ni Nani?”
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Desemba 15
    • Mambo Mengi Kumhusu Yesu

      Ikiwa Yesu angezusha swali hilo leo, labda angeuliza hivi: “Wasomi wanasema mimi ni nani?” Tena, majibu yangekuwa kama ifuatavyo: Kuna maoni mengi mbalimbali. “Yesu amekuwa farasi ambaye ameendeshwa na watu tofauti-tofauti akielekezwa sehemu mbalimbali,” akasema David Tracy wa Chuo Kikuu cha Chicago. Katika karne iliyopita, wasomi wametumia njia tata za kuchunguza mambo ya kijamii na hekaya wakitafuta kujua Yesu alikuwa nani. Baada ya kutumia njia hizo, wanafikiri Yesu alikuwa nani?

      Wasomi fulani wanadai kwamba Yesu anayetajwa katika historia alikuwa nabii Myahudi aliyehubiri kuhusu mwisho wa ulimwengu, na kuwasihi watu watubu. Hata hivyo, hawamwiti Mwana wa Mungu, Mesiya, au Mkombozi. Wengi hutilia shaka simulizi la Biblia kuhusu asili yake ya kimbingu na kufufuliwa kwake. Wengine humwona Yesu kuwa mtu wa kawaida tu ambaye maisha na mafundisho yake mazuri yalichochea kuanzishwa kwa dini kadhaa ambazo baadaye zilipata kuwa sehemu ya Ukristo. Kama ilivyotajwa katika kichapo Theology Today, bado wengine humwona Yesu kuwa ‘mchambuzi, mtu mwenye hekima aliyetangatanga, mkulima asiyejulikana vizuri; msimamzi wa jamii, mshairi mwasi-mila mwenye kuchambua utengamano wa jamii, au mchochezi stadi aliyeeleza maoni yake miongoni mwa wanakijiji wa hali ya chini wenye hasira ambao walikuwa tayari kutenda jeuri.’

  • Yule Yesu Halisi
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Desemba 15
    • Je, Ni Shaka Zenye Msingi?

      Lakini je, kweli twaweza kuamini masimulizi ya vitabu vya Injili kumhusu Yesu? Je, yanasimulia kuhusu yule Yesu halisi? Frederick F. Bruce, aliyekuwa profesa wa uchambuzi na ufafanuzi wa Biblia kwenye Chuo Kikuu cha Manchester, Uingereza, alisema: ‘Kwa kawaida haiwezekani kuthibitisha kihistoria kila habari kuhusu maandishi ya kale, yawe yamo katika Biblia au la. Inatosha kuwa na uhakika kwamba mwandishi ni mtu mwenye kutumainika; tukiwa na uhakika huo, basi inaelekea sana kwamba habari zake ni za kweli. Agano la Kale ni lenye kutegemeka kihistoria kwa sababu Wakristo walilipokea kama kichapo “kitakatifu.”’

      Baada ya kuchunguza zile zinazoonekana kuwa shaka kuhusu Yesu anayetajwa katika vitabu vya Injili, James R. Edwards, profesa wa dini kwenye Chuo cha Jamestown, North Dakota, Marekani, aliandika hivi: ‘Twaweza kuthibitisha kwa uhakika kwamba Injili zina uthibitisho mbalimbali na ulio muhimu kuhusu Yesu. Jinsi ambavyo Injili humtambulisha Yesu hupatana na akili kwa sababu hivyo ndivyo alivyokuwa hasa. Injili zimehifadhi kwa uaminifu maoni ya wafuasi wake kumhusu, kwamba kwa kweli alitumwa na Mungu na kupewa mamlaka ya kuwa Mwana na Mtumishi wa Mungu.’a

      Kumtafuta Yesu

      Namna gani vichapo vingine mbali na Biblia vinavyomtaja Yesu? Vinachanganuliwa jinsi gani? Vitabu vya Tacitus, Suetonius, Josephus, Pliny Mchanga, na waandishi wengine wa kale vina marejezo mengi kumhusu Yesu. Kichapo The New Encyclopædia Britannica (1995) chasema hivi kuhusu vichapo hivyo: ‘Masimulizi hayo yanathibitisha kwamba katika nyakati za kale hata wapinzani wa Ukristo hawakutilia shaka kamwe kuwepo kwa Yesu, ambako kulitiliwa shaka mara ya kwanza bila sababu zenye msingi mwishoni mwa karne ya 18, katika karne ya 19, na mwanzoni mwa karne ya 20.’

      Inasikitisha kwamba wasomi wa kisasa wamekosa kumfahamu vizuri Yesu “halisi” au “anayetajwa katika historia” kwa sababu ya kukisiakisia kusiko na msingi, shaka zisizofaa, na nadharia zisizo na msingi. Kwa njia fulani, wao ndio wenye hatia ya kutunga hadithi zisizo za kweli huku wakiwalaumu kimakosa waandishi wa Injili. Wengine wana hamu nyingi sana ya kupata umashuhuri tu na kuwa wa kwanza kuanzisha nadharia mpya, hivi kwamba hawachunguzi kwa unyofu uthibitisho wa kuwepo kwa Yesu. Kwa kufanya hivyo, wanabuni “Yesu” ambaye ni wa kuwaziwa tu na wasomi.

      Wale wanaotaka kumfahamu yule Yesu halisi wanaweza kufanya hivyo kwa kujifunza Biblia. Luke Johnson, profesa wa Agano Jipya na asili ya Ukristo kwenye Shule ya Theolojia ya Candler katika Chuo Kikuu cha Emory, adai kwamba utafiti mwingi kuhusu Yesu anayetajwa katika historia hupuuza malengo ya Biblia. Asema kwamba huenda ikapendeza kuchunguza mambo ya kijamii, kisiasa, kibinadamu, na kitamaduni yanayohusu maisha ya Yesu na kipindi alichoishi. Hata hivyo, anaendelea kusema kwamba, “lengo la Maandiko ni kufafanua zaidi utu wa Yesu,” ujumbe wake, na daraka analotimiza akiwa Mkombozi, badala ya kutambulisha yule ambaye wasomi wanamwita Yesu anayetajwa katika historia.

  • Yule Yesu Halisi
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Desemba 15
    • [Sanduku/Picha katika ukurasa wa 6]

      Yale Ambayo Wengine Wamesema

      ‘Ninamwona Yesu wa Nazareti kuwa mmojawapo wa walimu wakuu zaidi ambao wamepata kuishi ulimwenguni. . . . Nitawaambia Wahindu kwamba maisha yenu hayatakuwa kamili msipojifunza mafundisho ya Yesu.’—Mohandas K. Gandhi, The Message of Jesus Christ.

      “Mtu aliye mbunifu sana, kamili, mwenye kutegemeka, mkamilifu, mwenye ubinadamu na hata hivyo anayezidi sana wanadamu wote kwa ukuu, haiwezekani alikuwa mtu bandia wala mtu wa kuwaziwa tu. . . . Ingebidi kuwe na mtu mwenye uwezo kuliko Yesu ili kumbuni Yesu.”—Philip Schaff, History of the Christian Church.

      “Kwamba wanaume wachache wa kawaida wangeweza kwa kizazi kimoja kubuni mtu mwenye nguvu na mwenye uvutano mwingi kadiri hiyo, mwenye maadili ya hali ya juu kadiri hiyo na mtu mwenye kuonyesha ubinadamu sana kwa kadiri hiyo, ungekuwa muujiza wenye kustaajabisha mno zaidi ya wowote ulioandikwa katika Gospeli.”—Will Durant, Ceasar and Christ.

      ‘Huenda likaonekana kuwa jambo lisiloeleweka kwamba mtu wa kuwaziwa tu ambaye hajawahi kuishi angeweza kufaulu kuanzisha kundi la kidini linalopatikana ulimwenguni pote kwani watu wengi sana wamejaribu kufanya hivyo wakashindwa.’—Gregg Easterbrook, Beside Still Waters.

      “Nikiwa mwanahistoria wa fasihi ninasadiki kabisa kwamba Gospeli si hekaya hata kidogo. Si za ubunifu vya kutosha kuwa hekaya. . . . Kuna mambo mengi tusiyoyajua kuhusu maisha ya Yesu, na watu wenye kubuni hekaya hawangekosa kueleza habari zote kuhusu maisha yake.”—C. S. Lewis, Mere Christianity.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki