Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yule Yesu Halisi
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Desemba 15
    • Je, Ni Shaka Zenye Msingi?

      Lakini je, kweli twaweza kuamini masimulizi ya vitabu vya Injili kumhusu Yesu? Je, yanasimulia kuhusu yule Yesu halisi? Frederick F. Bruce, aliyekuwa profesa wa uchambuzi na ufafanuzi wa Biblia kwenye Chuo Kikuu cha Manchester, Uingereza, alisema: ‘Kwa kawaida haiwezekani kuthibitisha kihistoria kila habari kuhusu maandishi ya kale, yawe yamo katika Biblia au la. Inatosha kuwa na uhakika kwamba mwandishi ni mtu mwenye kutumainika; tukiwa na uhakika huo, basi inaelekea sana kwamba habari zake ni za kweli. Agano la Kale ni lenye kutegemeka kihistoria kwa sababu Wakristo walilipokea kama kichapo “kitakatifu.”’

      Baada ya kuchunguza zile zinazoonekana kuwa shaka kuhusu Yesu anayetajwa katika vitabu vya Injili, James R. Edwards, profesa wa dini kwenye Chuo cha Jamestown, North Dakota, Marekani, aliandika hivi: ‘Twaweza kuthibitisha kwa uhakika kwamba Injili zina uthibitisho mbalimbali na ulio muhimu kuhusu Yesu. Jinsi ambavyo Injili humtambulisha Yesu hupatana na akili kwa sababu hivyo ndivyo alivyokuwa hasa. Injili zimehifadhi kwa uaminifu maoni ya wafuasi wake kumhusu, kwamba kwa kweli alitumwa na Mungu na kupewa mamlaka ya kuwa Mwana na Mtumishi wa Mungu.’a

  • Yule Yesu Halisi
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Desemba 15
    • “Mtu aliye mbunifu sana, kamili, mwenye kutegemeka, mkamilifu, mwenye ubinadamu na hata hivyo anayezidi sana wanadamu wote kwa ukuu, haiwezekani alikuwa mtu bandia wala mtu wa kuwaziwa tu. . . . Ingebidi kuwe na mtu mwenye uwezo kuliko Yesu ili kumbuni Yesu.”—Philip Schaff, History of the Christian Church.

      “Kwamba wanaume wachache wa kawaida wangeweza kwa kizazi kimoja kubuni mtu mwenye nguvu na mwenye uvutano mwingi kadiri hiyo, mwenye maadili ya hali ya juu kadiri hiyo na mtu mwenye kuonyesha ubinadamu sana kwa kadiri hiyo, ungekuwa muujiza wenye kustaajabisha mno zaidi ya wowote ulioandikwa katika Gospeli.”—Will Durant, Ceasar and Christ.

      ‘Huenda likaonekana kuwa jambo lisiloeleweka kwamba mtu wa kuwaziwa tu ambaye hajawahi kuishi angeweza kufaulu kuanzisha kundi la kidini linalopatikana ulimwenguni pote kwani watu wengi sana wamejaribu kufanya hivyo wakashindwa.’—Gregg Easterbrook, Beside Still Waters.

      “Nikiwa mwanahistoria wa fasihi ninasadiki kabisa kwamba Gospeli si hekaya hata kidogo. Si za ubunifu vya kutosha kuwa hekaya. . . . Kuna mambo mengi tusiyoyajua kuhusu maisha ya Yesu, na watu wenye kubuni hekaya hawangekosa kueleza habari zote kuhusu maisha yake.”—C. S. Lewis, Mere Christianity.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki