-
Thamini Daraka la Pekee la Yesu Katika Kusudi la MunguMnara wa Mlinzi—2008 | Desemba 15
-
-
“Kuhani Mkuu”
15. Daraka la Yesu akiwa Kuhani Mkuu ni tofauti jinsi gani na la wanaume wengine wote ambao walitumikia wakiwa makuhani wakuu?
15 Wakati uliopita wanaume wengi walitumikia wakiwa makuhani wakuu, hata hivyo daraka la Yesu akiwa Kuhani Mkuu ni la pekee sana. Jinsi gani? Paulo anaeleza hivi: “Yeye hahitaji kila siku, kama wale makuhani wakuu wanavyofanya, kutoa dhabihu, kwanza kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe kisha kwa ajili ya zile za watu: (kwa maana yeye alifanya hilo mara moja kwa wakati wote alipojitoa mwenyewe;) kwa maana Sheria huweka rasmi kuwa makuhani wakuu watu walio na udhaifu, lakini neno la kiapo rasmi lililokuja baada ya Sheria humweka rasmi Mwana, ambaye amekamilishwa milele.”—Ebr. 7:27, 28.b
16. Kwa nini dhabihu ya Yesu ni ya pekee sana?
16 Yesu alikuwa mwanadamu mkamilifu, aliyelingana kabisa na Adamu kabla hajatenda dhambi. (1 Kor. 15:45) Kwa hiyo, Yesu alikuwa ndiye mwanadamu pekee ambaye angeweza kutoa dhabihu kamilifu, aina ya dhabihu ambayo haikuhitaji kutolewa tena na tena. Chini ya Sheria ya Musa, dhabihu zilitolewa kila siku. Hata hivyo, dhabihu zote hizo na huduma za kikuhani zilikuwa kivuli tu cha yale ambayo Yesu angetimiza. (Ebr. 8:5; 10:1) Kwa hiyo, cheo cha Yesu akiwa Kuhani Mkuu ni cha pekee kwa kuwa anaweza kutimiza mengi zaidi kuliko wale makuhani wakuu wengine na atatumikia daima katika daraka lake.
17. Kwa nini tunapaswa kuthamini daraka la Yesu akiwa Kuhani wetu Mkuu, na tunaweza kufanya hivyo jinsi gani?
17 Tunahitaji huduma za Yesu akiwa Kuhani Mkuu ili tuweze kuwa na msimamo mzuri mbele za Mungu. Tuna Kuhani Mkuu mzuri ajabu kama nini! Paulo aliandika hivi: “Tuna kuhani mkuu, si mtu ambaye hawezi kuusikitikia udhaifu wetu, bali yeye ambaye amejaribiwa katika mambo yote kama sisi wenyewe, lakini bila kuwa na dhambi.” (Ebr. 4:15) Kwa kweli, tukithamini jambo hilo tutachochewa ‘tusiishi tena kwa ajili yetu wenyewe, bali kwa ajili ya yeye aliyekufa kwa ajili yetu.’—2 Kor. 5:14, 15; Luka 9:23.
-
-
Thamini Daraka la Pekee la Yesu Katika Kusudi la MunguMnara wa Mlinzi—2008 | Desemba 15
-
-
◼ Kuhani Mkuu. (Ebr. 7:27, 28) Yesu alikuwa ndiye mwanadamu pekee ambaye angeweza kutoa dhabihu kamilifu, dhabihu ambayo haikuhitaji kutolewa tena na tena. Anaweza kusafisha dhambi zetu na kutuweka huru kutokana na kifo kinachosababishwa na dhambi.
-