Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ukosefu wa Makao—Suluhisho Ni Nini?
    Amkeni!—2005 | Desemba 8
    • Mashahidi wa Yehova wanasadiki kwamba njia yenye matokeo zaidi ya kuwasaidia watu wenye tatizo la ukosefu wa makao ni kuwafundisha watu njia bora zaidi ya maisha. Hilo linamaanisha kufuata mashauri bora zaidi, yaani, mashauri yanayotolewa na Muumba wa wanadamu. Hakuna mtu mwingine yeyote anayestahili zaidi kutoa mashauri kama hayo. Mashauri yake yanawasaidia watu kuepuka matatizo ambayo husababisha ukosefu wa makao. Pia yanawasaidia watu wanyoofu wasio na makao kutatua tatizo hilo. Bila shaka, kusoma Biblia tu hakuwezi kuondoa matatizo yote tunayokabili. Hata hivyo, Biblia inaweza kuwasaidia watu waache mazoea mabaya yanayowafanya watumie pesa nyingi, wajiheshimu kwa kiasi fulani, na waishi maisha mazuri.

      Watu wengi wamepoteza makao yao kwa sababu ya mambo mbalimbali kama vile kutumia vibaya kileo na dawa za kulevya, uhalifu, matatizo ya kifedha, au kuvunjika kwa familia. Biblia hutoa mashauri yanayofaa kuhusu mambo hayo yote. Kufuata mashauri hayo kumewasaidia mamilioni ya watu wabadili mtazamo wao kuhusu maisha na kuboresha utu wao. Bila shaka, kufuata tu mashauri ya Biblia hakutatatua matatizo yote yanayohusiana na ukosefu wa makao. Kwa sasa, misiba ya asili, magonjwa, kuenea kwa umaskini, uraibu, na matatizo kama hayo, yanahitaji kutatuliwa kwa njia tofauti. Ingawa Mashahidi wa Yehova hufanya yote wawezayo kuwasaidia watu wanaoteseka kwa sababu ya matatizo hayo, wanatambua kwamba ni Mfanyi wa wanadamu pekee anayeweza kutatua matatizo hayo kabisa.

  • Ukosefu wa Makao—Suluhisho Ni Nini?
    Amkeni!—2005 | Desemba 8
    • Mashahidi wa Yehova wanajitahidi kuwatolea watu msaada wa kiroho wanaohitaji sasa hivi. Wanatamani kuwapa wengine uangalifu wenye upendo ambao Yesu alipendekeza. (Mathayo 22:36-39) Kuwahangaikia wengine kwa njia hiyo huwachochea wawasaidie wale ambao wamepoteza makao yao kwa sababu ya misiba ya asili.a

      Mashahidi wanatambua kwamba haiwezekani kusaidia kila mtu. Jacek, kutoka Poland, ambaye anaishi katika makao ya manispaa ya watu wasio na makao anasema hivi kuhusu watu wasio na makao: “Baadhi yao ni wakali au hutumia dawa za kulevya. Wengine huchukia kuzungumzia mambo ya kidini, wakifikiri kwamba Mungu hapendezwi nao. Lakini kuna wale wanaosikiliza Neno la Mungu.” Kwa mfano, Jacek amefanya hivyo. Ameanza kujifunza mengi zaidi kuhusu mafundisho ya Biblia.

      Mtu mwingine asiye na makao ambaye alisikiliza Neno la Mungu ni Roman anayeugua UKIMWI ambaye ameishi barabarani hadi hivi majuzi. Anasema: “Nilipowasili kwenye kituo kinachotoa Huduma za Kijamii, sikujua kwamba Mashahidi wa Yehova walikuwa wakikutana karibu na mahali hapo. Punde si punde wakaanza kuzungumza nami barabarani na kunieleza kwamba Mungu husikia vilio vya kuomba msaada vya watu wasio na makao. Pia walinikaribisha kwenye mmoja wa mikutano yao.”—Zaburi 72:12, 13

      Mambo aliyosikia yalimwathirije? “Nilijifunza kwamba ninaweza kuishi milele katika Paradiso duniani na kwamba mimi ni mwenye thamani machoni pa Mungu. Nikiwa na marafiki wengi wapya na wenye kujali, niliacha kufikiria hali yangu na nikaanza kubadili utu wangu. Kwa sababu ya kumpenda Mungu, niliacha kuvuta sigara na katika sala nikaazimia kwamba ningetembea katika njia ya uadilifu.”

      Roman alifanya maendeleo ya kiroho na baada ya muda akabatizwa na kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Kwa msaada wa waamini wenzake na wenye mamlaka, aliweza kuhamia makao yanayofaa. Roman anasema hivi kwa furaha: “Nina furaha isiyo na kifani moyoni. Nimemkaribia Mungu mwenye upendo ambaye amefanya maisha yangu yawe na kusudi tena. Alinipa ndugu na dada wazuri sana na pia makao mazuri!”

      Wakati Ujao wa Watu Wasio na Makao

      Mashahidi wa Yehova hujitahidi kuwaonyesha huruma jirani zao wote, kutia ndani watu wasio na makao. Wanatamani kuwaeleza wengine kweli za Biblia kuhusu wakati ujao mzuri zaidi, kweli ambazo hata sasa zinaweza kubadili maisha.—Yohana 8:32.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki