-
NgonoKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Biblia inasema nini kuhusu ngono kati ya watu wa jinsia moja?
Rom. 1:24-27: “Kwa kupatana na tamaa za mioyo yao, Mungu aliwaacha katika uchafu, ili miili yao ivunjiwe heshima kati yao . . . Mungu aliwaacha katika hamu za ngono yenye kufedhehesha, kwa maana wanawake wao walibadili matumizi yao wenyewe ya asili kuwa yale yaliyo kinyume cha asili; na vivyo hivyo pia hata wanaume waliacha matumizi ya asili ya mwanamke na kuwakiana tamaa kali katika uchu wao kuelekeana wao wenyewe, wanaume kwa wanaume, wakitenda mambo machafu na kupokea ndani yao wenyewe malipo kamili, yaliyostahili kosa lao.”
1 Tim. 1:9-11: “Sheria huwekwa, si kwa ajili ya mtu mwadilifu, bali kwa ajili ya watu wenye kuasi sheria na watundu, wasiomwogopa Mungu na watenda-dhambi, . . . waasherati, wanaume wanaolala na wanaume, . . . na jambo lingine lolote linalopinga fundisho lenye afya kulingana na habari njema yenye utukufu ya Mungu mwenye furaha.” (Linganisha na Mambo ya Walawi 20:13.)
Yuda 7: “Sodoma na Gomora na majiji yaliyoyazunguka, baada ya hayo . . . kwenda kufuatilia mwili kwa ajili ya matumizi yasiyo ya asili, . . . yamewekwa mbele yetu kuwa kielelezo cha kuonya kwa kupatwa na adhabu ya hukumu ya moto wa milele.” (Jina Sodoma ndilo msingi wa neno la Kiingereza “sodomy,” ambalo kwa kawaida humaanisha tendo la ngono kati ya watu wa jinsia moja. Linganisha na Mwanzo 19:4, 5, 24, 25.)
Wakristo wa kweli wanawaonaje wale ambao wamekuwa na zoea la kufanya ngono na watu wa jinsia moja?
1 Kor. 6:9-11: “Wala waasherati, wala waabudu-sanamu, wala wazinzi, wala wanaume wanaowekwa kwa ajili ya makusudi yasiyo ya asili, wala wanaume wanaolala na wanaume . . . hawataurithi ufalme wa Mungu. Na bado wengine wenu mlikuwa hivyo. Lakini mmeoshwa mkawa safi, lakini mmetakaswa, lakini mmetangazwa kuwa waadilifu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo na kwa roho ya Mungu wetu.” (Bila kujali matendo hayo ya zamani, ikiwa sasa watu wanayaacha matendo yao machafu ya zamani, wafuate viwango vya uadilifu vya Yehova, na kuwa na imani katika uandalizi wake wa msamaha wa dhambi kupitia Kristo, wanaweza kupata msimamo safi mbele za Mungu. Baada ya kujirekebisha, wanaweza kukaribishwa katika kutaniko la Kikristo.)
Wakristo wa kweli wanajua kwamba watu ambao kweli wanataka kumpendeza Yehova wanaweza kuzishinda hata tamaa mbaya zenye nguvu, kutia ndani zile ambazo huenda zikawa za kurithiwa au zile zinazohusisha visababishi vya kimwili au vya kimazingira. Watu fulani kwa asili wanakasirika upesi. Labda zamani walikuwa wepesi kukasirika; lakini kuyajua mapenzi ya Mungu, tamaa ya kutaka kumpendeza, na msaada wa roho yake huwawezesha kujizuia. Huenda mtu akawa mlevi, lakini, akiwa na kichocheo kinachofaa, anaweza kuacha kunywa na hivyo aepuke kuwa mlevi. Vivyo hivyo, huenda mtu akahisi kuvutiwa sana na watu wa jinsia yake, lakini akitii shauri la Neno la Mungu, anaweza kubaki safi bila kufanya ngono na watu wa jinsia yake. (Ona Waefeso 4:17-24.) Yehova haturuhusu tuendelee kufikiri kwamba mwenendo mbaya ni sawa tu; kwa fadhili lakini kwa uthabiti yeye hutuonya juu ya matokeo naye huwapa msaada mwingi wale wanaotaka ‘kuvua utu wa zamani pamoja na mazoea yake, na kujivika utu mpya.’—Kol. 3:9, 10.
-
-
NgonoKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Mtu Akisema—
‘Mna maoni gani kuhusu ngono kati ya watu wa jinsia moja?’
Unaweza kujibu hivi: ‘Ni maoni yanayosemwa katika Biblia. Ninaamini kwamba yale ambayo inasema ni muhimu zaidi kuliko maoni ya mwanadamu yeyote, kwa sababu Biblia hutupa mawazo ya Muumba wa wanadamu. (1 Kor. 6:9-11) Utaona kwamba baadhi ya watu hawa waliokuja kuwa Wakristo, hapo zamani walifanya ngono na watu wa jinsia yao. Lakini kwa sababu ya kumpenda Mungu, na kwa msaada wa roho yake, walibadilika.’
Au unaweza kusema: ‘Ninapojibu hilo, ninaweza kusema nimeona kwamba watu wengi ambao hawaoni ngono kati ya watu wa jinsia moja kuwa jambo la aibu hawakubali Biblia kuwa ni Neno la Mungu. Je, una maoni gani kuhusu Biblia?’ Mtu huyo akidai kwamba anaiamini Biblia, unaweza kuongezea: ‘Ngono kati ya watu wa jinsia moja si suala jipya. Biblia inasema maoni ya Yehova Mungu yasiyobadilika kwa kutumia maneno yaliyo wazi sana. (Labda tumia habari katika ukurasa wa 235, 236.)’ Mtu huyo akionyesha shaka juu ya kuwako kwa Mungu au juu ya Biblia, unaweza kuongezea: ‘Ikiwa hakuna Mungu, ni jambo linalopatana na akili kwamba hatuwezi kuwajibika kwake nasi tunaweza kuishi kama tunavyopenda. Kwa hiyo swali ni hili, Je, kuna Mungu na je, mimi nipo kwa sababu aliniumba [pia, unaweza kusema, Je, Biblia iliongozwa na roho ya Mungu]? (Tumia habari kutoka ukurasa wa 215-221 au 32-42.)’
-