Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Tumaini Zuri Zaidi kwa Ajili ya Nafsi
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Agosti 1
    • Hata hivyo, Wakristo wa kweli hawako bila tumaini kwa habari ya kifo cha nafsi. Ufufuo wa Lazaro ni mojapo masimulizi mengi ya Biblia yanayotuonyesha waziwazi tumaini la kweli, la Kimaandiko kwa ajili ya nafsi zilizokufa—ufufuo. Biblia hufundisha juu ya aina mbili tofauti za ufufuo. Kwa wanadamu walio wengi sana wanaolala kaburini, wawe ni waadilifu au wasio waadilifu, kuna tumaini la ufufuo kwenye uhai wa milele katika Paradiso hapa duniani. (Luka 23:43; Yohana 5:28, 29; Matendo 24:15) Kwa kikundi kidogo ambacho Yesu alirejezea kuwa “kundi [lake] dogo,” kuna ufufuo kwenye uhai usioweza kufa wakiwa viumbe wa roho mbinguni. Hao, wanaotia ndani mitume wa Kristo, watatawala pamoja na Kristo Yesu juu ya wanadamu na kuwarudisha kwenye ukamilifu.—Luka 12:32; 1 Wakorintho 15:53, 54; Ufunuo 20:6.

  • Tumaini Zuri Zaidi kwa Ajili ya Nafsi
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Agosti 1
    • Ni afadhali kama nini kuwa na tumaini linalotegemea kweli, badala ya uwongo au falsafa za kibinadamu. Ni afadhali kama nini kuwa na uhakika kwamba wapendwa wetu waliokufa wamo kaburini bila ufahamu badala ya kuhangaikia mahali ambapo nafsi isiyoweza kufa imeenda! Kulala huko kwa wafu hakupaswi kutuhofisha au kutushusha moyo. Kwa njia fulani, twaweza kuona wafu kuwa katika mahali salama pa kupumzikia. Kwa nini salama? Kwa sababu Biblia hutuhakikishia kwamba wafu wanaopendwa na Yehova wako hai katika maana ya pekee. (Luka 20:38) Wako hai katika kumbukumbu lake. Hilo ni wazo lenye kufariji sana kwa sababu kumbukumbu lake halina mipaka. Ana hamu ya kurudisha kwenye uhai mamilioni yasiyohesabika ya wanadamu wapendwa na kuyapa fursa ya kuishi milele juu ya dunia iliyo paradiso.—Linganisha Ayubu 14:14, 15.

      Ile siku tukufu ya ufufuo itakuja, kwa kuwa ni lazima ahadi zote za Yehova zitimizwe. (Isaya 55:10, 11) Ebu fikiria unabii huu ukitimizwa: “Lakini wafu wako waishi, miili yao itainuka tena. Wale walalao katika dunia wataamka na kupiga kelele kwa shangwe; kwa kuwa umande wako ni umande wa nuru ya kumetameta, na dunia itawazaa tena wale waliokufa zamani.” (Isaya 26:19, The New English Bible) Kwa hiyo wafu wanaolala kaburini wako salama sawa na kitoto kilicho katika tumbo la uzazi la mama yacho. Wako karibu ‘kuzaliwa,’ kurudishwa kwenye uhai juu ya dunia iliyo paradiso!

      Ni tumaini gani ambalo lingeweza kuwa zuri zaidi kuliko hilo?

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki