Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Lidia—Mwabudu wa Mungu Mkaribishaji-Wageni
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Septemba 15
    • Lidia—Mwabudu wa Mungu Mkaribishaji-Wageni

      TANGU nyakati za kale, watumishi wa Mungu wa kweli wamejitofautisha kwa ukaribishaji-wageni wao. (Mwanzo 18:1-8; 19:1-3) Ufafanuliwao kuwa “upendo wa, upendezi kwa ajili ya, au fadhili kuelekea wageni,” ukaribishaji-wageni utokanao na moyo mweupe hata leo ni ishara ya Ukristo wa kweli. Kwa kweli, huo ni takwa kwa wote ambao wangemwabudu Mungu kwa kukubalika.—Waebrania 13:2; 1 Petro 4:9.

      Mtu mmoja aliyeonyesha ukaribishaji-wageni katika njia ionyeshayo kielelezo kizuri alikuwa Lidia. Yeye ‘aliwashurutisha’ wamishonari Wakristo waliokuwa wakizuru Filipi wakae nyumbani kwake. (Matendo 16:15) Ingawa Lidia anatajwa kifupi tu katika Maandiko, machache yasemwayo juu yake yaweza kuwa kitia-moyo kwetu. Vipi? Lidia alikuwa nani? Twajua nini kumhusu?

  • Lidia—Mwabudu wa Mungu Mkaribishaji-Wageni
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Septemba 15
    • ‘Alitushurutisha Tuje’

      Kabla ya kukutana na Lidia, huenda wamishonari hao walilazimika kuridhika na malazi waliyopata kwa gharama zao wenyewe. Lakini alifurahia kuweza kuwatolea malazi ya badala. Jambo la kwamba alilazimika kuwashurutisha ladokeza kwamba Paulo na waandamani wake walikataa kwa kiasi fulani. Kwa nini? Paulo alitaka ‘kuitoa injili bila gharama, bila kutumia kwa utimilifu uwezo wake’ na kutokuwa mzigo wa kulemea kwa yeyote. (1 Wakorintho 9:18; 2 Wakorintho 12:14) Lakini Luka aongeza hivi: “Hata alipokwisha kubatizwa, yeye na nyumba yake, akatusihi, akisema, Kama mmeniona kuwa mwaminifu kwa Bwana, ingieni nyumbani mwangu mkakae. Akatushurutisha.” (Matendo 16:15) Lidia alipendezwa zaidi na kuwa mwaminifu kwa Yehova, na kutoa ukaribishaji-wageni yaonekana kulikuwa uthibitisho wa imani yake. (Linganisha 1 Petro 4:9.) Ni kielelezo kizuri kama nini! Je, sisi pia hutumia mali zetu ili kuendeleza masilahi ya habari njema?

      Ndugu Katika Filipi

      Paulo na Sila walipowekwa huru kutoka gerezani baada ya kisa kilichohusisha kijakazi aliyepagawa na roho waovu, walirudi nyumbani kwa Lidia, walikopata ndugu fulani. (Matendo 16:40) Huenda ikawa waamini katika kutaniko la Filipi lililotoka kufanyizwa karibuni walitumia nyumba ya Lidia kuwa mahali pa kukutania pa kawaida. Yafaa kufikiri kwamba nyumba yake iliendelea kuwa kitovu cha utendaji wa kitheokrasi katika jiji hilo.

      Ukaribishaji-wageni mchangamfu wa kwanza ulioonyeshwa na Lidia ulithibitika kuwa sifa ya kutaniko lote. Licha ya umaskini wao, pindi kadha wa kadha Wafilipi walimtumia Paulo vitu alivyohitaji, na mtume huyo alikuwa mwenye shukrani.—2 Wakorintho 8:1, 2; 11:9; Wafilipi 4:10, 15, 16.

      Lidia hatajwi katika barua ambayo Paulo aliwatumia Wafilipi karibu mwaka wa 60-61 W.K. Maandiko hayafunui lililompata baada ya matukio yaliyosimuliwa katika Matendo sura ya 16. Hata hivyo, huo mtajo mfupi wa mwanamke huyo mwenye kutokeza hutufanya tutake ‘kufuata mwendo wa ukaribishaji-wageni.’ (Warumi 12:13, NW) Sisi ni wenye shukrani kama nini kwa kuwa na Wakristo kama Lidia miongoni mwetu! Roho yao huchangia sana kufanya makutaniko yawe yenye uchangamfu na yenye urafiki, kwa utukufu wa Yehova Mungu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki