-
“Yeye Ni Mwenye Hekima Moyoni”—Lakini MnyenyekevuMkaribie Yehova
-
-
c Biblia inaonyesha kwamba subira ni kinyume cha kiburi. (Mhubiri 7:8) Subira ya Yehova inathibitisha hata zaidi kwamba yeye ni mnyenyekevu.—2 Petro 3:9.
-
-
“Yeye Ni Mwenye Hekima Moyoni”—Lakini MnyenyekevuMkaribie Yehova
-
-
11, 12. Abrahamu alipataje kuelewa unyenyekevu wa Yehova?
11 Yehova yu tayari pia kuwasikiliza wanadamu wasiokamilika ambao wanataka sana kumweleza mahangaiko yao. Kwa mfano, Yehova alipomwambia Abrahamu kwamba alikusudia kuharibu Sodoma na Gomora, mwanamume huyo mwaminifu alishtuka. Abrahamu akasema, “Hasha usifanye hivyo,” kisha akaongezea hivi: “Mhukumu ulimwengu wote asitende haki?” Alimwuliza Yehova kama angeacha miji hiyo iwapo ingekuwa na watu 50 wenye haki. Yehova alimhakikishia kwamba Hangeiangamiza. Lakini Abrahamu akamwuliza swali hilo tena na tena, na kupunguza idadi hiyo hadi 45, kisha 40, na kuendelea. Abrahamu aliendelea kuuliza maswali hadi idadi hiyo ilipofikia kumi licha ya Yehova kumhakikishia kwamba hangeangamiza miji hiyo. Huenda Abrahamu hakufahamu vyema rehema ya Yehova. Vyovyote iwavyo, kwa subira Yehova alimruhusu rafiki na mtumishi wake Abrahamu aeleze mahangaiko yake.—Mwanzo 18:23-33.
12 Ni wanadamu wangapi wenye akili, na wenye elimu ambao wangemsikiliza kwa subira mtu asiye na akili nyingi sana?c Mungu wetu alionyesha unyenyekevu mkubwa kwa kumsikiliza Abrahamu kwa makini sana.
-