Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Umewahi Kuwa na Mapendeleo ya Utumishi? Je, Unaweza Kutumikia Tena?
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Agosti 15
    • Ikiwa ulipoteza pendeleo kwa sababu ulifanya kosa fulani, huenda ukajiuliza ikiwa Yehova na ndugu zako Wakristo wanaweza kukusamehe kikweli na kusahau jambo hilo. Ikiwa unahisi hivyo, hebu sasa chunguza kisa cha Mfalme Manase wa Yuda. “Alifanya kwa kiasi kikubwa yale yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova, na kumtia uchungu.” (2 Fal. 21:6) Hata hivyo, kufikia wakati wa kifo chake, Manase alikuwa mwanamume mwaminifu, akitawala kama mfalme. Hilo lilifanyika jinsi gani?

      Mwishowe, Manase alikubali nidhamu. Baada ya kupuuza maonyo, Yehova aliwaruhusu Waashuru wamshambulie, wakamfunga kwa pingu na kumpeleka uhamishoni huko Babiloni. Akiwa huko, Manase ‘aliutuliza uso wa Yehova Mungu wake, akaendelea kujinyenyekeza sana kwa sababu ya Mungu wa mababu zake. Naye akaendelea kusali kwake Yeye.’ Kutubu kutoka moyoni kulimchochea achukue hatua ili kurekebisha mambo, na Manase akasamehewa.—2 Nya. 33:12, 13.

  • Umewahi Kuwa na Mapendeleo ya Utumishi? Je, Unaweza Kutumikia Tena?
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Agosti 15
    • Kubali nidhamu. Huenda mwanzoni Manase alihisi kwamba hakustahili adhabu kali aliyopewa. Hata hivyo, aliikubali, akatubu, na kuacha mwenendo wake mbaya. Hata iwe unahisi jinsi gani kuhusu nidhamu ambayo umepewa, ‘jinyenyekeze machoni pa Yehova, naye atakuinua.’—1 Pet. 5:6; Yak. 4:10.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki