Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Kwa Hilo Wote Watajua Kwamba Nyinyi Ni Wanafunzi Wangu”
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Kielelezo kimoja cha upendo huo ukiwa katika tendo ulionwa kufuatia Kimbunga Andrew, kilichoathiri pwani ya Florida, Marekani, katika saa za asubuhi mapema siku ya Jumatatu, Agosti 24, 1992. Kufuatia kimbunga hicho, watu 250,000 waliachwa bila makao. Maelfu ya Mashahidi wa Yehova walikuwa miongoni mwa majeruhi. Karibu na mara hiyo Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova lilitenda kwa kuagiza halmashauri ya kutoa misaada na ikapanga kutoa fedha za msaada. Waangalizi Wakristo katika eneo lililoathiriwa waliwasiliana upesi na Mashahidi mmoja-mmoja ili kujua mahitaji yao na kutoa msaada. Jumatatu asubuhi, siku ya kimbunga hicho, tayari Mashahidi walioko umbali wa mamia ya kilometa katika South Carolina walikuwa wamepeleka kilori kilichopakiwa jenereta, misumeno-umeme, na maji ya kunywa kuelekea sehemu ya msiba. Siku ya Jumanne, mamia ya wenye kujitolea wa kutoka nje ya mji waliwasili pamoja na ugavi zaidi ambao ulikuwa umetolewa kuwa upaji, ili kusaidia ndugu wenyeji katika kurekebisha Majumba ya Ufalme na makao ya faragha. Mwanamke asiye Shahidi aliyeishi karibu na Jumba la Ufalme alisema hivi kuhusu jitihada za kutoa misaada: “Kwa kweli huu lazima uwe ndio upendo wa Kikristo ambao Biblia husema juu yao.”

  • “Kwa Hilo Wote Watajua Kwamba Nyinyi Ni Wanafunzi Wangu”
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • [Sanduku katika ukurasa wa 712]

      “Mashahidi Watunza Walio Wao—Na Wengineo”

      Chini ya kichwa kikuu hicho, “The Miami Herald” liliripoti juu ya jitihada za kutoa msaada za Mashahidi wa Yehova katika Florida Kusini kufuatia uharibifu ulioletwa na Kimbunga Andrew mnamo Agosti 1992. Makala hiyo ilisema: “Hakuna yeyote katika Homestead anayefunga mlango Mashahidi wa Yehova wanapobisha juma hili—hata ingawa wangali na milango ya kufunga. Mashahidi wenye kujitolea kama 3,000 kotekote nchini wamekutana kwenye sehemu ya msiba, kwanza kusaidia walio wao, kisha kusaidia wengineo. . . . Tani za chakula na ugavi karibu 150 zimepitishwa katika kituo cha kutoa misaada kwenye Jumba la Kusanyiko katika magharibi mwa Wilaya ya Broward hadi kwenye Majumba ya Ufalme mawili katika eneo la Homestead. Kutoka kwa majumba hayo, wafanyakazi huenda kwenye eneo tofauti kila asubuhi ili kurekebisha makao yaliyobomolewa ya ndugu Mashahidi. . . . Jiko la muda hutokeza milo kwa ajili ya watu kama 1,500, mara tatu kila siku. Na si soseji tu na maandazi. Wenye kujitolea huandaliwa mkate uliookwa, lasanya iliyotayarishwa, saladi zilizochanganywa na krimu, supu, chapati na tosti-mayai—zote zikitayarishwa kwa vitu vilivyotolewa upaji.”—Agosti 31, 1992, ukurasa 15A.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki