-
NyongezaTengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
-
-
ikiwa unastahili kubatizwa. Unaweza kuanza kupitia maswali haya katika funzo lako la kibinafsi la kawaida.
Unapojitayarisha kwa ajili ya mazungumzo hayo, tenga wakati wa kusoma na kutafakari Maandiko yaliyotajwa au kunukuliwa. Unaweza kuandika maelezo yako katika kitabu hiki au mahali pengine. Unaweza kutumia maelezo hayo pamoja na kitabu hiki utakapokuwa ukizungumza na wazee. Ukishindwa kuelewa swali lolote, usisite kumwomba yule anayekufundisha Biblia au mzee yeyote akusaidie.
Utakapokuwa ukizungumza na wazee, usihisi kwamba unahitaji kujibu maswali haya kwa kutoa maelezo marefu yenye mambo mengi. Jibu rahisi, la moja kwa moja na kwa maneno yako mwenyewe litafaa. Kwa maswali yaliyo mengi, ingefaa kurejelea andiko moja au mawili yanayoonyesha msingi wa Kimaandiko wa jibu lako.
Ikiwa bado hujapata ujuzi wa kutosha wa mafundisho ya msingi ya Biblia, wazee watapanga upate msaada ili uweze kuyafahamu Maandiko vizuri na kuyaeleza kwa maneno yako mwenyewe ili ustahili kubatizwa wakati mwingine.
[Taarifa kwa wazee wa kutaniko: Maagizo kuhusu mazungumzo pamoja na wale wanaotaka kubatizwa yanapatikana kwenye ukurasa wa 208-212.]
-
-
Sehemu ya 1: Mafundisho ya KikristoTengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
-
-
MASWALI KWA AJILI YA WALE WANAOTAKA KUBATIZWA
Sehemu ya 1: Mafundisho ya Kikristo
Kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova kumekusaidia kuijua kweli. Bila shaka, mambo uliyojifunza yamekusaidia kuwa na uhusiano mzuri pamoja na Mungu na kukupatia tumaini la baraka na uzima wa wakati ujao katika dunia paradiso chini ya Ufalme wa Mungu. Imani yako katika Neno la Mungu imeimarishwa, na tayari umepata baraka nyingi kwa kushirikiana na kutaniko la Kikristo. Umejionea jinsi Yehova anavyoshughulika na watu wake leo.—Zek. 8:23.
Unapojiandaa kwa ajili ya ubatizo, utafaidika kwa kupitia mafundisho ya msingi ya Kikristo pamoja na wazee wa kutaniko. (Ebr. 6:1-3) Yehova na aendelee kukubariki unapojitahidi kuendelea kumjua, na akupe thawabu aliyoahidi.—Yoh. 17:3.
-