-
Kwa Nini Ninalazimika Kuwa Mgonjwa Sana?Amkeni!—1997 | Aprili 22
-
-
JASON alipokuwa na umri wa miaka 13, alikusudia moyoni mwake kwamba wakati fulani baadaye angetumikia akiwa mhudumu wa wakati wote katika Betheli, makao makuu ya ulimwengu ya Mashahidi wa Yehova katika Brooklyn, New York. Alijitengenezea sanduku la mbao na aliliita sanduku la Betheli. Alianza kukusanya vitu ndani yalo ambavyo alifikiri vingekuwa vyenye kufaa atakapoanza utumishi wake wa Betheli.
Lakini, miezi mitatu tu baada ya kutimiza miaka 18, Jason aligunduliwa kuwa ana maradhi ya Crohn—kasoro ya tumbo yenye maumivu makali yenye kudumu. “Yaliniangamiza kabisa,” akumbuka. “Nilichoweza tu kufanya ni kumpigia simu baba yangu kazini na kulia. Nilijua kwamba, angalau ndoto yangu ya kwenda Betheli imepatwa na kizuizi.”
-
-
Kwa Nini Ninalazimika Kuwa Mgonjwa Sana?Amkeni!—1997 | Aprili 22
-
-
“Uwapo kijana, wahisi ukiwa na nguvu za kuweza kufanya jambo lolote,” asema Jason, aliyetajwa mwanzoni. “Kisha kwa ghafula, uwapo mgonjwa sana watambua kwamba huna nguvu za kuweza kufanya jambo lolote. Wahisi kwamba umekuwa mzee kwa usiku mmoja, kwani walazimika kupunguza shughuli zako.” Naam, ni vigumu kupambana na vizuizi vipya.
Jason alipata kwamba tatizo jingine kubwa huja wakati wengine washindwapo kuelewa hali yako. Jason ana kile kiwezacho kuitwa “ugonjwa usioonekana.” Sura yake ya nje haionyeshi tatizo lake la ndani. “Mwili wangu haumeng’enyi chakula kama unavyopaswa,” aeleza Jason, “Hivyo ninalazimika kula mara kwa mara na ninakula chakula kingi zaidi ya wengine. Hata hivyo, bado mimi ni mwembamba. Pia, pindi nyingine mimi huchoka sana kiasi cha kushindwa kuwa macho wakati wa mchana. Lakini watu husema maneno yaonyeshayo kwamba mimi ni mwenye kujiachilia sana au mvivu. Wao husema maneno kama vile: ‘Wajua kwamba unaweza kufanya zaidi. Lakini hata hujaribu!’”
Jason ana ndugu na dada wachanga ambao hawaelewi mara zote kwa nini hawezi kufanya mambo ambayo alikuwa anafanya zamani, kama vile kuwapeleka kucheza mpira. “Lakini najua kwamba ikiwa nitaumia,” asema Jason, “yaweza kuchukua majuma kadhaa ili kupona. Waelekea kulinganisha maumivu yangu na yao na kusema, ‘Yeye apiga kite tu ili aangaliwe.’ Maumivu yao makubwa zaidi labda ni kuteguka kwa mguu, hivyo hawawezi kuwazia maumivu yangu yakoje hasa.”
Ikiwa ugonjwa wako unakuwa mzigo kwa familia, waweza kupambana na hatia. Wazazi wako pia waweza kuhisi hatia. “Wazazi wangu wote wawili waamini kwamba wamenirithisha tatizo hilo,” asema Jason. “Kwa kawaida watoto huweza kujirekebisha kwa tatizo baada ya kuukubali uhalisi wa tatizo hilo. Lakini wazazi wana wakati mgumu zaidi. Wao huniomba msamaha kwa kurudia-rudia. Ninalazimika kufanya yote niwezayo nyakati zote ili kujaribu kutuliza hisia zao za hatia.”
-