Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Magonjwa ya Kuambukiza Katika Karne ya 20
    Amkeni!—1997 | Novemba 22
    • Maradhi Mapya Yaliyotambulika

      Bado maradhi mengine ni mageni, yakitambulika tu hivi majuzi. Shirika la WHO hivi majuzi lilitaarifu: “Katika miaka 20 iliyopita, angalau maradhi mapya 30 yametokea kutisha afya ya mamia ya mamilioni ya watu. Mengi ya maradhi hayana tiba, ponyo au chanjo na uwezekano wa kuyazuia au kuyadhibiti ni mdogo.”

      Kwa kielelezo, fikiria HIV na UKIMWI. Karibu miaka 15 tu iliyopita hayakuwa yakijulikana, sasa yataabisha watu katika kila kontinenti. Kwa sasa, karibu watu wazima milioni 20 wameambukizwa na HIV, na zaidi ya milioni 4.5 wameshikwa na UKIMWI. Kulingana na ripoti ya Human Development Report 1996, sasa UKIMWI ni kisababishi kinachoongoza cha vifo vya watu wazima walio na umri wa chini ya miaka 45 katika Ulaya na Amerika Kaskazini. Ulimwenguni pote, watu wapatao 6,000 wanaambukizwa kila siku—mmoja kwa kila sekunde 15. Makadirio ya wakati ujao yadokeza kwamba idadi ya visa vya UKIMWI itaendelea kuongezeka kwa haraka. Kufikia mwaka wa 2010, matarajio ya maisha katika mataifa ya Afrika na Asia yaliyoathiriwa zaidi na UKIMWI yanatarajiwa kupungua kufikia miaka 25, kulingana na shirika moja la msaada la Marekani.

      Je, UKIMWI ni maradhi ya kipekee, au mlipuko wa magonjwa mengine waweza kutokea na kusababisha maangamizi kama hayo au hata mabaya zaidi? Shirika la WHO lajibu: “Bila shaka, maradhi ambayo sasa hayajulikani lakini yenye uwezekano wa kuwa UKIMWI wa kesho waotea.”

  • Magonjwa ya Kuambukiza Katika Karne ya 20
    Amkeni!—1997 | Novemba 22
    • Maradhi Fulani Mapya ya Kuambukiza Tangu 1976

      Mahali Visa

      Vilipotokea

      Mwaka Kwanza

      Vilivyotambuliwa Jina la Maradhi au Kutambuliwa

      1976. Maradhi ya Legionnaires. Marekani

      1976. Cryptosporidiosis. Marekani

      1976. Homa ya kuvuja damu ya Ebola. Zaire

      1977. Virusi ya Hantaan. Korea

      1980. Mchochota wa Ini Aina ya D (Delta) Italia

      1980. Virusi ya Human T-cell lymphotropic 1 Japani

      1981. UKIMWI. Marekani

      1982. E. coli O157:H7. Marekani

      1986. Bovine spongiform encephalopathy*. Uingereza

      1988. Salmonella enteritidis PT4. Uingereza

      1989. Mchochota wa Ini Aina ya C. Marekani

      1991. Homa ya kuvuja damu ya Venezuela. Venezuela

      1992. Vibrio cholerae O139. India

      1994. Homa ya kuvuja damu ya Brazili. Brazili

      1994. Human and equine morbillivirus. Australia

      *Visa vya wanyama pekee.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki