-
Baraka au Laana—Vielelezo kwa Ajili Yetu LeoMnara wa Mlinzi—1996 | Juni 15
-
-
7. Twaweza kulindaje moyo wa kitamathali?
7 Twaweza kupingaje uharibifu wa moyo? Kwa kujifunza Neno la Mungu kwa bidii, tukiruhusu kweli zalo zipenyeze ndani ya akili zetu na mioyo yetu. (Warumi 12:1, 2) Bila shaka twapaswa kuhudhuria mikutano ya Kikristo kwa ukawaida. (Waebrania 10:24, 25) Kuhudhuria mikutano kwa kujikalia tu kungeweza kufananishwa na kupaka rangi mahali penye kutu. Hilo huenda likatuchangamsha kwa muda mfupi, lakini halitatui tatizo la msingi. Badala ya hivyo, kwa utayarishaji wa kimbele, kutafakari, na kushiriki kwa bidii katika mikutano, twaweza kwa juhudi nyingi kuondoa mambo yaletayo uharibifu ambayo huenda yakaendelea kukaa ndani ya moyo wetu wa kitamathali. Hilo litatusaidia kushikamana na Neno la Mungu na kutatuimarisha kuvumilia mitihani ya imani na kuwa “watimilifu bila kupungukiwa na neno.”—Yakobo 1:3, 4; Mithali 15:28.
Onyo Dhidi ya Uasherati
8-10. (a) Ni kielelezo gani cha kuonya kinachorejezewa kwenye 1 Wakorintho 10:8? (b) Maneno ya Yesu yanayopatikana kwenye Mathayo 5:27, 28 yaweza kutumiwaje kwa njia ya kunufaisha?
8 Katika kielelezo kifuatacho cha Paulo, tunashauriwa hivi: “Wala msifanye uasherati, kama wengine wao walivyofanya, wakaanguka siku moja watu ishirini na tatu elfu.”a (1 Wakorintho 10:8) Mtume alikuwa akirejezea wakati Waisraeli walipoinamia miungu isiyo ya kweli “wakaanza kuzini pamoja na wanawake wa Moabu.” (Hesabu 25:1-9) Ukosefu wa adili katika ngono unastahili kifo! Kuruhusu mawazo na tamaa zisizo za adili kuendelea bila kuzuiwa ni kama kuruhusu moyo “kuwa na kutu.” Yesu alitaarifu hivi: “Mmesikia kwamba imenenwa, Usizini; lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake.”—Mathayo 5:27, 28.
-
-
Baraka au Laana—Vielelezo kwa Ajili Yetu LeoMnara wa Mlinzi—1996 | Juni 15
-
-
Sawa na vile kutu huhitaji kuondolewa, acheni tuchukue hatua chanya ili kuondoa tamaa zisizofaa katika mioyo yetu
-