-
Ipinge “Roho ya Ulimwengu”Mnara wa Mlinzi—2008 | Septemba 15
-
-
1, 2. (a) Kwa nini ndege walikuwa wakiwekwa katika migodi huko Uingereza? (b) Wakristo wanakabili hatari gani?
MWAKA wa 1911, wenye mamlaka nchini Uingereza walitunga sheria ili kuokoa uhai wa wachimbaji wa migodi ya makaa ya mawe. Kila mgodi ulipaswa kuwa na ndege wawili wanaoitwa kurumbiza. Kwa nini? Ikiwa moto ungetokea katika mgodi, waokoaji wangewapeleka ndege hao chini ya ardhi. Ndege hao wadogo wanaweza kutambua gesi zenye sumu, kama vile kaboni monoksidi. Ikiwa hewa ingechafuliwa na gesi hizo, ndege hao wangeweza kuonyesha dalili za kwamba wanateseka, na hata kuanguka. Onyo hilo la mapema lilikuwa la maana. Kaboni monoksidi ni gesi isiyo na rangi, isiyo na harufu, na inayoua kwa kuzuia chembe nyekundu za damu zisipitishe oksijeni ndani ya mwili. Ikiwa waokoaji hao hawangeonywa, wangezimia na kufa bila kutambua kwamba wanapumua hewa yenye sumu.
2 Katika maana ya kiroho, Wakristo wanakabili hali kama ile iliyowakabili wachimbaji hao wa migodi. Jinsi gani? Yesu alipowapa wanafunzi wake mgawo wa kuhubiri habari njema ulimwenguni pote, alijua kwamba anawatuma katika eneo hatari, ambalo linatawaliwa na Shetani na roho ya ulimwengu. (Mt. 10:16; 1 Yoh. 5:19) Yesu aliwahangaikia sana wanafunzi wake hivi kwamba usiku uliotangulia kifo chake, alisali hivi kwa Baba yake: “Ninakuomba, si kwamba uwatoe ulimwenguni, bali uwalinde kwa sababu ya yule mwovu.”—Yoh. 17:15.
3, 4. Yesu aliwapa wanafunzi wake onyo gani, na kwa nini tupendezwe nalo?
3 Yesu aliwaonya wafuasi wake kuhusu hatari ambayo ingesababisha wasinzie na kufa kiroho. Maneno yake yanatuhusu sana, kwa kuwa tunaishi wakati wa umalizio wa mfumo wa mambo. Aliwahimiza wanafunzi wake hivi: “Endeleeni kukesha . . . ili mpate kufanikiwa kuponyoka mambo yote hayo yaliyokusudiwa kutukia, na kusimama mbele ya Mwana wa binadamu.” (Luka 21:34-36) Hata hivyo, inatia moyo kwamba Yesu aliahidi pia kuwa Baba yake angewapa roho takatifu ambayo ingewakumbusha mambo na kuwasaidia kuwa macho na imara.—Yoh. 14:26.
-
-
Ipinge “Roho ya Ulimwengu”Mnara wa Mlinzi—2008 | Septemba 15
-
-
Tambua Dalili Ambazo Zinakuonya Mapema
9-11. Ni dalili gani zinazotuonya kwamba huenda tunaongozwa na roho ya ulimwengu?
9 Wachimbaji wa migodi huko Uingereza waliotajwa mwanzoni, walitumia ndege ili kutambua mapema ikiwa kuna gesi zenye sumu. Ikiwa mchimbaji angeona ndege akianguka, alijua kwamba anahitaji kuchukua hatua ya haraka ili kuokoka. Vivyo hivyo, kwa upande wa kiroho, ni dalili gani zinazoweza kutuonya mapema kwamba tunaongozwa na roho ya ulimwengu?
10 Tulipoanza kujifunza kweli za Neno la Mungu na kujiweka wakfu kwa Yehova, huenda tulisoma Biblia kwa bidii. Labda tulisali kwa bidii mara nyingi. Na tulifurahia kuhudhuria mikutano ya kutaniko, tukiona kila mkutano kuwa wenye kuburudisha kiroho, kama ambavyo maji yanavyomburudisha mtu mwenye kiu. Mazoea hayo yalitusaidia kuikataa na kuendelea kuipinga roho ya ulimwengu.
11 Je, bado tunajitahidi kusoma Biblia kila siku? (Zab. 1:2) Je, tunasali mara nyingi na kwa moyo wote? Je, tunapenda mikutano ya kutaniko na kuhudhuria yote kila juma? (Zab. 84:10) Au, je, tumeacha mengine kati ya mazoea hayo mazuri? Bila shaka, huenda tuna shughuli nyingi zinazochukua wakati na nguvu zetu, na huenda ikawa vigumu kuendelea kuwa na ratiba nzuri ya kiroho. Lakini ikiwa tumeacha mazoea fulani mazuri ambayo tulikuwa nayo, je, inawezekana kwamba sasa tunaongozwa na roho ya ulimwengu? Je, tutajitahidi sana kusitawisha tena mazoea mazuri tuliyokuwa nayo?
-