-
Yehova Ni Bwana Wetu Mwenye Enzi Kuu!Mnara wa Mlinzi—2010 | Novemba 15
-
-
Drama hiyo inaweza kufananishwa na hali fulani ambayo inaweza kuwa katika nchi fulani. Kwa upande mmoja, kuna serikali halali ambayo inadumisha utaratibu. Na kwa upande mwingine, kuna kikundi cha wahalifu ambao wanatawala kwa udanganyifu, jeuri, na mauaji. Kikundi hicho haramu kinatatiza serikali halali na pia kinajaribu ushikamanifu wa raia wote kwa serikali hiyo.
3 Kuna hali kama hiyo katika ulimwengu wote. Kuna serikali halali ya “Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova.” (Zab. 71:5) Lakini sasa wanadamu wanatishwa na kikundi cha wahalifu kinachoongozwa na “yule mwovu.” (1 Yoh. 5:19) Kikundi hicho kinatatiza serikali halali ya Mungu na kinajaribu ushikamanifu wa watu wote kuelekea utawala wake halali.
-
-
Yehova Ni Bwana Wetu Mwenye Enzi Kuu!Mnara wa Mlinzi—2010 | Novemba 15
-
-
Ni nini ambacho kimetukia baada ya karne nyingi kupita? Shetani ameanzisha kikundi chenye nguvu cha wahalifu. Mwishowe, Yehova atamharibu Ibilisi na kikundi hicho, na kuthibitisha waziwazi kwamba Mungu ana haki ya kutawala. Yehova Mungu alikuwa na hakika kabisa kuwa matokeo yangekuwa mazuri hivi kwamba alitabiri hilo wakati uasi ulipotokea katika Edeni.—Mwa. 3:15.
-
-
Yehova Ni Bwana Wetu Mwenye Enzi Kuu!Mnara wa Mlinzi—2010 | Novemba 15
-
-
13. Tunaweza jinsi gani kuepuka kuharibiwa pamoja na maadui wa Yehova?
13 Ili tuepuke kuharibiwa pamoja na maadui wa Mungu, ni lazima tuthibitishe ushikamanifu wetu kwa enzi kuu ya Yehova. Tunaweza kufanya hivyo jinsi gani? Kwa kuendelea kujitenga na utawala wa kihalifu wa Shetani na kukataa kuogopeshwa na watumishi wake. (Isa. 52:11; Yoh. 17:16; Mdo. 5:29)
-